Mke wa kiongozi wa upinzani nchini Uganda aliye chini ya ulinzi Kizza Besigye, Jumapili amesema ana wasiwasi kuhusu afya yake, ikiwa karibu wiki moja baada ya mgombea huyo wa zamani wa urais kuanza mgomo wa kula.
Baadhi ya Wazungu wa Afrika Kusini, Jumamosi walionyesha kumuunga mkono Rais Donald Trump, kwa kukusanyika katika Ubalozi wa Marekani mjini Pretoria kudai wao ni waathirika wa ubaguzi wa rangi na serikali yao wenyewe.
Wanajeshi wa Russia, wameongeza kasi ya mashambulizi yao mashariki mwa Ukraine, jeshi la Kyiv, limesema Jumapili, huku afisa wa NATO akitabiri kuwa Moscow itaongeza kasi na nguvu ya mashambulizi yake wakati mazungumzo ya kumaliza vita yanakaribia.
Katika mkutano wa kilele wa Umoja wa Afrika uliofanyika Addis Ababa, Ethiopia, viongozi wa Afrika wamemchagua Waziri wa Mambo ya Nje wa Djibouti, Mahmoud Ali Youssouf, kuwa Mwenyekiti mpya wa Tume ya Umoja wa Afrika (AUC).
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres, Jumamosi amesema dola ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo iheshimiwe na kuepusha vita vya kikanda, katika mkutano wa Umoja wa Afrika, siku moja baada ya wapiganaji wanaoungwa mkono na Rwanda kuuteka mji mkuu wa pili wa jimbo la DRC.
Umoja wa Ulaya, (EU) Jumamosi umesema unatakari kwa dharura njia za kukabiliana na ongezeko la mashambulizi ya waasi mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, baada ya vikosi vinavyoungwa mkono na Rwanda kuuteka mji mkubwa wa pili.
Hamas imewaachilia huru mateka wengine watatu Jumamosi kwa mabadilishano na wafungwa wa Kipalestina huku sitisho tete la mapigano likitekelezwa licha ya mivutano wa karibuni.
Watu wengi wanatuhumu polisi kwa kufanya vitendo hivyo lakini bado haijathibitishwa ni nani aliyehusika na utekaji huo.
Inaelezwa kuwa safari ya ndege ya Mahan Air ya Iran kuelekea Beirut ilifutwa kabla ya kupaa kwa sababu Lebanon haikutoa ruhusa ya kutua.
Papa Francis mwenye umri wa miaka 88 amekuwa Papa tangu 2013 na amekuwa akisumbuliwa na matatizo ya kiafya mara kadhaa.
Senegal imeanza kuzalisha aina mbalimbali za mafuta katika kiwanda chake cha kusafisha mafuta karibu na mji mkuu wa Dakar, kampuni iliyosafisha mafuta hayo ilisema Alhamisi.
Hamas Alhamisi ilisema itawaachilia mateka watatu zaidi wa Israel mwishoni mwa juma kama ilivyopangwa kwa kubadilishana na wafungwa wa Kipalestina.
Pandisha zaidi