Mazungumzo hayo ni ya kwanza kutangazwa hadharani kati ya waasi na mamlaka ya Senegal iliyochaguliwa mwezi Machi mwaka jana
Viongozi hao walifanya mazungumzo wakati Rais wa Marekani Donald Trump akishinikiza kufikiwa makubaliano ya kumaliza vita vya Ukraine
Mazungumzo na Israel kupitia wapatanishi kuhusu hatua zijazo katika makubaliano ya kusitisha mapigano yana masharti ya kuwaachilia wafungwa wa Kipalestina kama ilivyokubaliwa, afisa wa Hamas Basem Naim alisema Jumapili.
Rais wa zamani wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo Joseph Kabila Jumapili alisema uongozi mbaya wa mrithi wake, Rais Felix Tshisekedi umechangia pakubwa kwa kuzidisha mzozo mashariki mwa nchi.
Marekani na Ukraine Jumapili zimesema zinakaribia kufikia makubaliano kwa Kyiv Kuipa Washington Sehemu kubwa ya madini yake nadra kama malipo ya fidia kwa mabilioni ya dola ya zana za kijeshi ambazo Marekani iliipa Ukraine kujihami dhidi ya vita vya Russia.
Waconservative nchini Ujerumani wameshinda uchaguzi wa taifa Jumapili lakini uchaguzi huo wenye kura zilizosambaratika umekipa chama cha mrengo mkali wa kulia cha Alternative for Germany (ADF) matokeo yake mazuri kwa kupata nafasi ya pili.
Vikosi vya akiba vya Sudan (RSF) na washirika wake Jumapili wamekubaliana kuunda serikali ya pamoja, licha ya onyo kwamba hatua hiyo inaweza kuisambaratisha zaidi nchi hiyo iliyoharibiwa na vita.
Wapiga kura wa Ujerumani wanachagua serikali mpya katika uchaguzi wa Jumapili uliotawaliwa na wasiwasi kuhusu kudorora kwa miaka mingi kwa uchumi mkubwa zaidi wa Ulaya, shinikizo la kuzuia uhamiaji na kutokuwa na uhakika juu ya mustakabali wa Ukraine na muungano wa Ulaya na Marekani.
Waziri wa ulinzi wa Israel, Jumapili amesema wanajeshi wataendelea kubaki katika sehemu za Ukingo wa Magharibi unaokaliwa na walozwezi ambapo Israel imefanya mashambulizi ya wiki nzima, huku ikisema inazidisha uchunguzi wake katika eneo la Palestina.
Myanmar na mshirika wake wa karibu Russia, walitia saini mkataba wa ushirikiano wa uwekezaji katika eneo maalum la kiuchumi la Dawei, ikiwa ni pamoja na ujenzi wa bandari na kiwanda cha kusafisha mafuta, Wizara ya Maendeleo ya Uchumi ya Russia, imesema Jumapili.
Papa Francis, Jumapili alikuwa na fahamu lakini bado anapokea mtiririko wa juu wa oksijeni ya ziada kufuatia tatizo la kupumua na kuongezewa damu, kwani bado yuko katika hali mbaya kwa maambukizo tata ya mapafu, Vatican imesema.
Kremlin Jumapili imesifu mazungumzo kati ya Rais wa Marekani, Donald Trump, na Rais wa Russia, Vladimir Putin, ikiwaita “marais wawili makini sana” na kuapa kuwa kamwe haitaachilia eneo lililotwaliwa mashariki mwa Ukraine.
Pandisha zaidi