Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Marco Rubio Jumatano ametangaza kwamba Marekani inapanga kuunga mkono Guatemala na miradi mipya ya miundombinu pamoja na kuondolewa ushuru kwenye misaada ya kigeni ili kuimarisha ushirika wa Marekani na taifa hilo la Amerika ya Kati.
Mashirika ya Umoja wa Mataifa yanayoshughulikia wakimbizi na uhamiaji kwa pamoja Jumatano yameelezea wasi wasi wao kuhusu mpango wa Pakistan wa kuanza mchakato mpya wa kurejesha halaiki ya wahamiaji wa Afghanistan pamoja na waomba hifadhi.
Karibu watu 70 wameuwawa na wengine 50 kujeruhiwa kufuatia mapigano ya saa 24 kati ya wapiganaji wa Islamic State na vikosi vya eneo la Somalia la Puntland.
Washirika wa Marekani pamoja na mahasimu wake wote Jumatano wameshutumu pendekezo la rais wa Marekani Donald Trump kwamba Marekani ichukue udhibiti wa Gaza
China imesema kwamba ipo tayari kushirikiana na Umoja wa Ulaya kukabiliana na changamoto zinazoukumba ulimwengu.
Serikali ya muungano wa kitaifa ya Afrika Kusini inayumba yumba kutokana na tofauti kati ya vyama tanzu vinavyounda serikali, lakini rais Cyril Ramaphosa amesema serikali hiyo ni thabithi.
Rais wa Marekani Donald Trump amesema anataka Marekani kuchukua umiliki wa Gaza, hatua inayovuka matamshi yake ya kuwalazimisha wapalestina kuondoka katika eneo eneo lililokumbwa na mapigano na kuhamia nchi jirani za Jordan na Misri.
Marekani imeufahamisha rasmi Umoja wa Mataifa kwamba imesitisha ufadhili wake kwa kikosi kinachoungwa mkono na Umoja wa Mataifa ambacho kilikuwa na jukumu la kupambana na magenge yanayojaribu kudhibiti mji mkuu wa Haiti, Umoja wa Mataifa ulisema Jumanne.
Takriban watu 10 Jumanne wameuwawa kwenye ufyatulianaji wa risasi kwenye kituo kimoja cha elimu kati kati mwa Sweden akiwemo mshambuliaji, maafisa wa polisi wamesema.
Rais wa Marekani Donald Trump ameendelea kusisitiza mpango wake wa kuondolewa kwa Wapalestina kutoka Gaza wakati akiwa mwenyeji wa Waziri Mkuu wa Israel Benjamini Netanyahu huko White House Jumanne.
Wachambuzi wa mambo wanasema kwamba Kundi la wanamgambo la Sudan -RSF limeanza kupoteza nguvu dhidi ya jeshi la taifa kutokana na makosa ya mikakati, ugomvi wa ndani kati ya viongozi wake na kupungua vifaa.
Rubio alikuwa nchini El Salvador kwa mazungumzo na Rais Nayib Bukele na alitangaza kuwa Bukele alikubali kupokea wahamiaji kutoka Marekani
Pandisha zaidi