Waasi wenye silaha waliwauwa zaidi ya raia 35, wakati wa shambulio dhidi ya vijiji kadhaa katika jimbo la Ituri, mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, usiku wa kuamkia leo, chifu wa kijiji kimoja amesema.
Rais Donald Trump Jumatatu alichukua hatua za kuongeza ushuru kwa kiasi kikubwa kwenye bidhaa za chuma na aluminum zinazoagizwa kutoka nje, na kufuta sheria iliyokuwa inaziruhusu Canada, Mexico, Brazil na nchi nyingine kuleta bidhaa hizo bila kulipa ushuru.
Umoja wa Mataifa Jumatatu ulisema umesitisha shughuli za kutoa misaada ya kibinadamu katika eneo ambalo ni ngome ya waasi wa Kihouthi wa Yemen baada ya waasi hao kuwashikilia wafanyakazi wanane wa Umoja huo.
Hali ilionekana kuwa tulivu Jumatatu kwa siku ya pili huko mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, baada ya viongozi wa SADC na Jumuia ya Afrika Mashariki kutoa wito wa sitisho la mapigamo kutokana na hofu kuwa mapigano yanaweza kuchochea mzozo mkubwa.
Hamas Jumatatu ilisema itachelewesha mpango wa kuwaachilia mateka zaidi katika Ukanda wa Gaza baada ya kuishtumu Israel kwa kukiuka makubaliano ya sitisho la mapigano ambayo kwa sasa yanakabiliwa na mzozo wake mkubwa zaidi tangu yaanze kutelezwa wiki tatu zilizopita.
Kiongozi wa shirika la Umoja wa Mataifa la Ukimwi UNAIDS Jumatatu amesema kwamba kesi mpya za maambuikizi ya HIV na Ukimwi huenda zikaongezeka kwa zaidi ya mara 6 kufikia 2029.
Huku shinikizo likiongezeka kwa Israel na Hamas kuongeza muda wa makubaliano ya kusitisha mapigano zaidi ya ilivyokua awali.
Kiwanda kinalenga kushindana na wazalishaji mafuta wa Ulaya wakati kinapoanza kufanya kazi kamili.
Uamuzi wa jaji Joseph N. Laplante wa New Hampshire umekuja baada ya hukumu mbili kama hizo kutolewa na majaji wengine wiki iliyopita.
Rais wa Marekani Donald Trump Jumapili alisema anaamini Marekani imepiga hatua katika mazungumzo ya kumaliza vita kati ya Russia na Ukraine, lakini hakutoa maelezo yoyote kuhusu mawasiliano kati yake na Rais Vladimir Putin.
Mamlaka nchini Libya zilipata karibu miili 50 kwenye makaburi mawili ya watu wengi katika jangwa la kusini mashariki mwa nchi hiyo, maafisa walisema Jumapili.
Sam Nujoma ambaye aliongoza mapambano ya miongo mitatu ya kupigania uhuru wa Namibia kutokea Afrika Kusini yenye ubaguzi wa rangi, amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 95, ofisi ya rais ilitangaza Jumapili.
Pandisha zaidi