Rais wa Cameroon Paul Biya atatizmiza umri wa miaka 92 kesho alhamisi na kuwa kiongozi mkongwe zaidi duniani.
Aliyekuwa mgombea wa urais nchini Uganda Dr. Kiiza Besigye yupo katika mgomo wa kutokula katika gereza la Luzira anakozuiliwa.
Vita vinavyoendelea mashariki mwa Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo vinatarajiwa kugubika mazungumzo kwenye kikao cha Umoja wa Afrika kinachotarajiwa kufanyika mwishoni mwa wiki hii ambapo mwenyekiti mpya wa umoja huo anatarajiwa kuchaguliwa.
Hali ya hewa ya theluji, na mvua ya barafu kali inatarajiwa kuendelea katika sehemu kadhaa Katikati mwa Marekani, Appalachinaa na majimbo ya yaliyo Katikati mwa Atlantic.
Waziri wa ulinzi wa Ukraine Rustem Umerov, amesema kwamba mkutano wa washirika wa nchi hiyo, unaofanyika Brussels leo Jumatano, unaangazia namna ya kutoa silaha zaidi kwa Ukraine, ikiwemo mifumo muhimu ya ulinzi.
Katibu mkuu wa umoja wa nchi za kiarabu Ahmed Aboul Gheit amekataa mpango wowote wa kuwahamisha wapalestina kutoka ukanda wa Gaza, akisema kwamba mpango kama huo hauwezi kukubalika.
Marc Fogel, mwalimu raia wa Marekani ambaye alikuwa anazuiliwa nchini Russia tangu Agosti 2021 kwa kuleta bangi inayoruhusiwa na madaktari nchini humo, aliachiliwa na Moscow Jumanne na alirejea nyumbani, White House ilitangaza.
Rais wa Sudan Kusini Salva Kiir amemfuta kazi mkuu wake mpya wa usalama na kumpandisha cheo mshirika wake kuwa makamu wa rais katika kile kinachohisiwa kuwa ni njia ya kumuandaa mrithi wake.
Waziri mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu ameonya kwamba makubaliano ya kusitisha mapigano na Hamas yatamalizika na mapigano makali kuanza tena huko Gaza ikiwa mateka zaidi wanaoshikiliwa na Hamas hawataachiliwa ifikapo Jumamosi.
Mapigano yalizuka Jumanne mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, siku tatu baada ya wito wa viongozi wa Afrika wa kusitisha mapigano na utulivu kwa muda mfupi katika mzozo huo.
Waasi wenye silaha waliwauwa zaidi ya raia 35, wakati wa shambulio dhidi ya vijiji kadhaa katika jimbo la Ituri, mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, usiku wa kuamkia leo, chifu wa kijiji kimoja amesema.
Rais Donald Trump Jumatatu alichukua hatua za kuongeza ushuru kwa kiasi kikubwa kwenye bidhaa za chuma na aluminum zinazoagizwa kutoka nje, na kufuta sheria iliyokuwa inaziruhusu Canada, Mexico, Brazil na nchi nyingine kuleta bidhaa hizo bila kulipa ushuru.
Pandisha zaidi