Aboul Gheit ameambia mkutano wa viongozi wa serikali duniani kwamba pendekezo la rais wa Marekani Donald Trump kuwahamisha karibu wapalestina Milioni 2 kutoka Gaza, utapelekea kanda hiyo nzima kuingia katika mgogoro usiomalizika na kuvuruga amani na utulivu.
Gheit amesema hauwezi kukubalika kabisa na umoja wa nchi za kiarabu ambao umepigania kwa maslahi yake kwa miaka 100.
Baada ya mazungumzo na rais Trump, Mfalme wa Jordan Abdullah II amesema kwamba alisisitiza msimamo wa nchi yake wa kupinga kuondolewa kwa wapalestina kutoka Gaza na ukingo wa magharibi.
Amesema kwamba lengo kubwa ni kujenga upya Gaza bila kuwaondoa wapalestina, Pamoja na kuhsughulikia hali ya kibinadamu ambayo ni mbaya sana.
Amezungumzia pia kile ametaja kuwa mchango muhimu wa Trumo katika kuhakikisha kwamba vita vinamalizika Gaza na kutaka Marekani Pamoja na washirika wengine kuhakikisha kwamba mapigano yanakoma kabisa.
Forum