Utafiti mpya umebaini kuwa ugonjwa wa kisukari aina ya Type 2 unaongezeka kwa kasi miongoni mwa baadhi ya watu barani Afrika Kusimi mwa Sahara kuliko ilivyodhaniwa.
Karibu watoto milioni 17 wameshindwa kwenda shule kwa kipindi cha miaka miwili. Wasichana wanakutana na hatari kubwa, ikiwemo ukatili wa kijinsia, biashara ya binadamu, na ndoa za kulazimishwa, kwa mujibu wa shirika la UNICEF.
Mashirika mawili ya Umoja wa Mataifa yanasema visa vya ugonjwa wa surua barani Ulaya vimeongezeka maradufu ikilinganishwa na mwaka uliopita, vikiongezeka hadi 127,000, idadi ya juu sana tangu mwaka 1997.
Mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa linalohudumia Watoto, UNICEF, Alhamisi alisema kwamba Watoto milioni 16 nchini Sudan wanateseka vibaya kutokana na vita vya wenyewe kwa wenyewe nchini humo.
Rais wa Russia Vladimir Putin ameunga mkono pendekezo la Marekani la kusitisha vita kati ya Russia na Ukraine lakini amesisitiza umuhimu wa kufanyia kazi maelezo yaliyomo katika pendekezo hilo.
Serikali ya Tanzania siku ya Alhamisi, imetangaza kumalizika kwa mlipuko wa ugonjwa wa Marburg baada ya siku 42 bila kuwepo na maambukizi mapya, hatua inayokidhi vigezo vya Shirika la Afya Duniani (WHO).
Rais wa Marekani Donald Trump Jumatano kwenye Ikulu ya Marekani amekutana na Waziri Mkuu wa Ireland Michael Martin wakati wakifanya mazungumzo mapana kuanzia tofauti za kibiashara hadi mzozo wa Gaza, ingawa wote waliahidi kuimarisha ushirikiano kati ya nchi hizo mbili.
Kiongozi mkuu wa Iran Ayatollah Ali Khamenei Jumatano ametupilia mbali wazo la kufanya mazungumzo na Marekani kuhusu mkataba wa nyuklia, baada ya kupokea barua kutoka kwa Rais Donald Trump ambaye alipendekeza mazungumzo hayo.
Jumuia ya maendeleo ya Afrika Mashariki Jumatano ilionya kwamba mapigano ya hivi karibuni nchini Sudan Kusini yanaipeleka nchi hiyo “kwenye hatari ya kurudi katika vita.”
Mazungumzo ya moja kwa moja kati ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na waasi wa M23 yataanza katika mji mkuu wa Angola tarehe 18 Machi, ofisi ya rais wa Angola ilisema Jumatano katika taarifa.
Vita vya kibiashara vya Marekani na Canada na Umoja wa Ulaya vilishika kasi Jumatano, huku Rais Donald Trump na washirika wa Marekani wakiwekeana ushuru mpya.
Pandisha zaidi