Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Machi 27, 2025 Local time: 05:27

Vita vya kibiashara kati ya Marekani na washirika wake vyashika kasi


Mfanyakazi katika kampuni ya North York Iron, inayouza bidhaa za chuma, huko Toronto Canada. Picha ya AFP
Mfanyakazi katika kampuni ya North York Iron, inayouza bidhaa za chuma, huko Toronto Canada. Picha ya AFP

Vita vya kibiashara vya Marekani na Canada na Umoja wa Ulaya vilishika kasi Jumatano, huku Rais Donald Trump na washirika wa Marekani wakiwekeana ushuru mpya.

Hatua ya Marekani ya kuweka ushuru wa asilimia 25 kwenye bidhaa za chuma na aluminum zinazoagizwa kutoka nchi 35, ikiwemo Canada na nchi 27 wanachama wa EU ilianza kutekelezwa Jumatano.

Marekani ilifuta pia msamaha wa awali wa kutolipa ushuru kwa bidhaa zinazoagizwa kutoka Argentina, Australia, Brazil, Uingereza, Japan, Mexico na Korea Kusini.

“Kwa maoni yangu, marekebisho haya ni muhimu ili kushughulikia ongezeko kubwa la uagizaji wa bidhaa za chuma za zile zinazozalishwa kutoka kwenye chuma, ambazo zinatishia kudhoofisha usalama wa Marekani,” Trump alisema wakati akitangaza ushuru huo.

Canada iliweka papo hapo ushuru mpya kwenye bidhaa zinazouzwa nje na Marekani zenye thamani ya dola bilioni 27, huku Umoja wa Ulaya ukitangaza hatua ya ulipizaji kisasi kwa kuweka ushuru kwenye bidhaa zinazozalishwa na viwanda vya Marekani na mazao ya ukilima nchini Marekani. Hatua hiyo mpya ya EU inahusu bidhaa za Marekani zenye thamani ya dola bilioni 28.

Forum

XS
SM
MD
LG