Rais wa Marekani Donald Trump Alhamisi amethibitisha kwamba utawala wake unafanya mashauriano na kundi la Hamas ambalo limeorodheshwa na Marekani ni la kigaidi.
Rais wa Marekani Donald Trump Alhamisi amechelewesha kwa wiki nne ushuru mpya wa asilimia 25 kwenye bidhaa nyingi kutoka Mexico na Canada kwa mauzo yake kuja Marekani.
Afrika Kusini inasema kwamba Marekani inajiondoa katika mpango wa kufadhili athari za mabadiliko ya hali ya hewa uliofikiwa na mataifa tajiri kuzisaidia nchi zinazoendelea kuachana na matumizi ya mkaa na kuanza kutumia nishati mbadala.
Hamas iliyotajwa kuwa kundi la kigaidi na Marekani ilisema Alhamisi kwamba vitisho kutoka kwa rais wa Marekani Donald Trump vinahimiza Israel iondoke kwenye makubaliano ya usitishaji mapigano huko Gaza.
Rais wa Marekani Donald Trump Jumatano amechelewesha kwa mwezi mmoja ushuru mpya wa asilimia 25 kwa magari kutoka Mexico na Canada wakati kukiwa na wasi wasi kwamba vita vya biashara na mataifa hayo jirani huenda vikawaumiza watengenezaji watatu wakubwa wa magari nchini Marekani.
Kwa mara ya kwanza katika historia ya sasa, Wamarekani wengi zaidi wanaamini kuwa nchi yetu inaelekea kwenye mwelekeo sahihi kuliko mwelekeo mbovu – katika rekodi ya kushangaza ya pointi 27 tangu siku ya uchaguzi.
Marekani imeweka bayana kwamba haitakuwa ikitoa mchango wa moja kwa moja kwa majukwaa ya Umoja wa Mataifa yakiwemo maendeleo endelevu pamoja na malengo mengine ya kimataifa ikijumuisha kutokomeza umaskini, katika upigaji kura kwenye Baraza Kuu la Umoja huo Jumanne.
Makamu wa Rais wa Marekani JD Vance ameweka wazi msimamo wa Marekani kuhusu kumaliza vita vya miaka mitatu kati ya Russia na Ukraine.
Wachambuzi wa siasa katika Umoja wa Ulaya wameonya kwamba itakuwa vigumu sana kwa umoja huo kuziba pengo la msaada wa ulinzi kwa Ukraine baada ya Rais wa Marekani Donald Trump kusitisha msaada huo kwa Kyiv na kuonyesha kuiunga mkono Russia.
Rais Donald Trump amekuwa wazi kwamba anazingatia amani, afisa wa ngazi ya juu wa utawala ameiambia VOA katika barua pepe.
Maelfu ya wakimbizi katika kambi hiyo ni watu wanaokimbia vita na ukame katika nchi jirani za Sudan Kusini, Ethiopia, Burundi na Congo
Pandisha zaidi