Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatatu, Machi 31, 2025 Local time: 08:06

Basi moja limelipuka na kuua watu wasiopungua 12 nchini Afrika kusini


Mfano wa ajali za basi nchini Afrika kusini ambazo zimetokea miaka ya nyuma. Picha inahusisha ajali huko De Doorns, Afrika kusini, Friday, March 15, 2013.
Mfano wa ajali za basi nchini Afrika kusini ambazo zimetokea miaka ya nyuma. Picha inahusisha ajali huko De Doorns, Afrika kusini, Friday, March 15, 2013.

Basi hilo lilibeba zaidi ya watu 50 waliokuwa wanakwenda kazini wakati lilipoanguka katika barabara yenye shughuli nyingi.

Basi moja lilipinduka katika eneo la Johannesburg karibu na uwanja mkuu wa ndege wa Afrika Kusini mapema Jumanne na kuua watu wasiopungua 12 maafisa wa mji huo wamesema huku wengine kadhaa wamejeruhiwa.

Basi hilo lilikuwa limebeba zaidi ya watu 50 waliokuwa wanakwenda kazini wakati lilipoanguka katika barabara yenye shughuli nyingi karibu na uwanja wa ndege wa kimataifa wa OR Tambo, maafisa wamesema. Watu 12 waliuawa na wengine 45 kujeruhiwa, wamesema katika taarifa. Tumeishiwa maneno.

Hili ni janga, afisa wa usafiri wa mji wa Ekurhuleni Andile Mngwevu alisema. Chanzo cha ajali hiyo hakijajulikana mara moja. Ililazimisha kufungwa kwa barabara kuu inayoelekea uwanja wa ndege. Picha kutoka eneo la tukio zililionyesha basi hilo.

Mmoja wa manusura wa ajali hiyo ameiambia televisheni ya Newzroom Afrika, kuwa inaonekana basi hilo lilikuwa likienda mwendo kasi.

Forum

XS
SM
MD
LG