Waziri Mkuu wa Ethiopia Abiy Ahmed amefanya ziara ya saa kadhaa mjini Mogadishu siku ya Alhamisi, kwa lengo la kuimarisha makubaliano dhaifu ya maridhiano kati ya nchi hizo mbili kufuatia ugomvi juu ya ushirikiano wake na jimbo lililojitenga la Somaliland.
Serikali ya Uganda imesema Jumatano kwamba mmoja wa wake na watoto watatu wa kiongozi wa uasi kutoka Uganda Joseph Kony wamerejeshwa Uganda kutoka Jamhuri ya Afrika ya Kati.
Mazungumzo hayo ni ya kwanza kutangazwa hadharani kati ya waasi na mamlaka ya Senegal iliyochaguliwa mwezi Machi mwaka jana
Viongozi hao walifanya mazungumzo wakati Rais wa Marekani Donald Trump akishinikiza kufikiwa makubaliano ya kumaliza vita vya Ukraine
Rais wa Tunisia Kais Saied siku ya Jumamosi alitoa wito kwa sheria inayosimamia benki kuu kufanyiwa marekebisho, na hivyo kuzua wasiwasi kwamba benki hiyo itapoteza uhuru wake na uingiliaji wa moja kwa moja wa serikali katika sera za fedha.
Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Marco Rubio na Rais wa Kenya William Ruto walihimiza kusitishwa kwa mapigano mara moja mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo wakati wa mazungumzo yao ya simu, Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani ilisema Ijumaa.
Makamu wa Rais wa Marekani JD Vance aliongoza Mkutano wa Siasa wa kihafidhina na vikao vingine muhimu vinavyohusu Cryptocurrency
Waziri wa mambo ya nje wa marekani Marco Rubio amezungumza na waziri wa mambo ya nje wa Angola Tete antoniuo jana kuhusu kubuni njia ya kuumaliza kwa amani mzozo wa mashariki mwa DRC , Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani imesema.
Serikali ya Kenya imkosolewa na mkuu wa jeshi la Sudan na baadhi ya wakosowaji wa nchi hiyo kwa kudai imefanya kitendo cha uhalifu wa kutowajibika kwa kuwaruhusu waasi wa kundi la wanamgambo wa Sudan RSF kukutana Nairobi na kupanga kutangaza serikali ya uhamishoni.
Mwanadiplomasia wa juu wa Marekani Marco Rubio hatohudhuria Mkutano wa mawaziri wa mambo ya nje wa G20 utakaofanyika Afrika kusini wiki hii huku kukiwa na mivutano inayoendelea baina ya mataifa hayo mawili.
Mashambulizi kutoka kwa kundi la kijeshi la Rapid Support Forces la Sudan yameua mamia ya raia wakiwemo watoto, kwenye jimbo la White Nile, maafisa wa serikali na makundi ya haki za binadamu wamesema Jumanne.
Rubio yupo Saudi Arabia huku kukiwa na upinzani kuhusu pendekezo la Rais wa Marekani Donald Trump la kuwaondoa Wapalestina kutoka Gaza
Pandisha zaidi