Kiongozi wa waasi wa Kihouthi wa Yemen, Ijuma amesema kundi hilo litarudia operesheni zake za kijeshi dhidi ya Israel, endapo Israel haitaondoa kizuizi cha misaada cha Gaza ndani ya siku nne.
Kimbunga Alfred kilidhoofika kitropiki Jumamosi kilipokaribia kuwa mvua na upepo uliovuma pwani ya mashariki mwa Australia ambapo mamia ya maelfu ya nyumba hazikuwa na umeme.
Maelfu ya wanawake waliandamana katika mitaa ya miji ya Uturuki Jumamosi kuadhimisha Siku ya Kimataifa ya Wanawake, kupinga ukosefu wa usawa na unyanyasaji dhidi ya wanawake.
Waumini wa kanisa katoliki wamekuwa na hisia mchanganyiko baada ya kusikia sauti ya Papa Francis leo Ijumaa, kwa mara ya kwanza tangu alipolazwa hospitali, mwezi Februari.
Serikali ya Thailand imesema Alhamisi kwamba inafanya majadiliano na maafisa wa serikali mbali mbali au maafisa wa balozi za nchi ambazo raia wao wamekwama kwenye mpaka kati ya Thailand na Myanmar.
Waziri wa Ulinzi wa Ufaransa Sebastien Lecornu alisema Alhamisi kwamba Ufaransa inashirikiana taarifa za kijasusi na Ukraine, hatua iliyofuatia baada ya Marekani kusema inapunguza ushirikiano wa kijasusi na Ukraine.
Hamas iliyotajwa kuwa kundi la kigaidi na Marekani ilisema Alhamisi kwamba vitisho kutoka kwa rais wa Marekani Donald Trump vinahimiza Israel iondoke kwenye makubaliano ya usitishaji mapigano huko Gaza.
Iran imekamilisha miezi miwili ya mazoezi makali ya kijeshi katika miongo kadhaa huku ikijaribu kuzuia uwezekano wa mashambulizi kutoka kwa mahasimu wake Israel na Marekani, watafiti wa usalama wameiambia VOA.
Wakati viongozi wa Umoja wa Ulaya wakijiandaa kwa mazungumzo ya dharura kuhusu misaada ya kijeshi baada ya utawala wa Trump kusitisha msaada wake kwa Ukraine, wataalam kadhaa wa Russia wanasema kuwa Moscow inajitahidi kuvuruga mshikamano wa Magharibi.
Canada, Mexico na China Jumanne wote wamesema kwamba wataweka ushuru wa majibu kwenye bidhaa kutoka Marekani kufutia hatua ya Rais wa Marekani Donald Trump ya kuweka ushuru mpya kwa bidhaa zao zinazoingia Marekani.
Rais wa serikali ya mpito ya Syria Ahmad al-Sharaa amewasili Cairo kuhudhuria mkutano wa viongozi wa nchi za Kiarabu.
Wachambuzi wa siasa katika Umoja wa Ulaya wameonya kwamba itakuwa vigumu sana kwa umoja huo kuziba pengo la msaada wa ulinzi kwa Ukraine baada ya Rais wa Marekani Donald Trump kusitisha msaada huo kwa Kyiv na kuonyesha kuiunga mkono Russia.
Pandisha zaidi