Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatano, Aprili 02, 2025 Local time: 18:16

Shambuzi la waasi laua wanavijiji 35 wa Ituri, DRC


Maafisa wa jeshi la FARDC nchini DRC.
Maafisa wa jeshi la FARDC nchini DRC.

Waasi wenye silaha waliwauwa zaidi ya raia 35, wakati wa shambulio dhidi ya vijiji kadhaa katika jimbo la Ituri, mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, usiku wa kuamkia leo, chifu wa kijiji kimoja amesema.

Kiongozi wa kundi la vijiji vya Djaiba katika eneo la Djugu, Jean Vianney, alisema wanamgambo wa CODECO walifanya shambulio hilo, lililoanza mwendo wa saa nane usiku, na kuwaua wakazi, na kuchoma moto nyumba zao.

“Tumehesabu watu zaidi ya 35 wamekufa asubuhi ya leo na msako unaendelea, alisema. Kiongozi wa jumuiya ya kiraia katika eneo hilo Jules Tsuba, alisema miili 49 ilikuwa imehesabiwa kufikia asubuhi ya Jumanne, na kwamba shughuli za uokoaji zilikuwa zinaendelea.

CODECO ni mojawapo ya makundi mengi ya waasi wanaopigania ardhi na rasilimali mashariki mwa Kongo.

Limeshutumiwa hapo awali na Umoja wa Mataifa kwa mashambulizi dhidi ya jamii nyingine, ikiwa ni pamoja na wafugaji wa kabila la Hema, ambayo yanaweza kuorodheshwa kama uhalifu wa kivita na uhalifu dhidi ya binadamu.

Wakazi wengi katika eneo la Djugu ni wa kabila la Hema.

Forum

XS
SM
MD
LG