Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres, Jumamosi amesema dola ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo iheshimiwe na kuepusha vita vya kikanda, katika mkutano wa Umoja wa Afrika, siku moja baada ya wapiganaji wanaoungwa mkono na Rwanda kuuteka mji mkuu wa pili wa jimbo la DRC.
Umoja wa Ulaya, (EU) Jumamosi umesema unatakari kwa dharura njia za kukabiliana na ongezeko la mashambulizi ya waasi mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, baada ya vikosi vinavyoungwa mkono na Rwanda kuuteka mji mkubwa wa pili.
Hamas imewaachilia huru mateka wengine watatu Jumamosi kwa mabadilishano na wafungwa wa Kipalestina huku sitisho tete la mapigano likitekelezwa licha ya mivutano wa karibuni.
Watu wengi wanatuhumu polisi kwa kufanya vitendo hivyo lakini bado haijathibitishwa ni nani aliyehusika na utekaji huo.
Inaelezwa kuwa safari ya ndege ya Mahan Air ya Iran kuelekea Beirut ilifutwa kabla ya kupaa kwa sababu Lebanon haikutoa ruhusa ya kutua.
Papa Francis mwenye umri wa miaka 88 amekuwa Papa tangu 2013 na amekuwa akisumbuliwa na matatizo ya kiafya mara kadhaa.
Senegal imeanza kuzalisha aina mbalimbali za mafuta katika kiwanda chake cha kusafisha mafuta karibu na mji mkuu wa Dakar, kampuni iliyosafisha mafuta hayo ilisema Alhamisi.
Hamas Alhamisi ilisema itawaachilia mateka watatu zaidi wa Israel mwishoni mwa juma kama ilivyopangwa kwa kubadilishana na wafungwa wa Kipalestina.
Rais wa Marekani Donald Trump Alhamisi alisema kwamba Ukraine itashirikishwa katika mazungumzo ya amani na Russia, licha ya kuwa Kyiv imesema ni mapema mno kuzungumza na Moscow kwenye mkutano wa usalama leo Ijumaa.
Nchi nyingi washirika wa wengi wa NATO Alhamisi zimeelezea uungaji mkono wa mpango wa kuongeza matumizi ya ulinzi, huku wakisisitiza haja ya Ukraine na mataifa mengine ya Ulaya kuwa sehemu ya mazungumzo ya kumaliza vita vya Russia dhidi ya Ukraine.
Watu wenye silaha mashariki mwa Kongo waliwabaka mamia ya watoto na kuwaandikisha wapiganaji watoto katika viwango ambavyo havijawahi kushuhudiwa, shirika la Umoja wa Mataifa la kuwahudumia watoto, UNICEF lilisema Alhamisi.
Mwandishi wa habari wa chombo cha habari dada cha VOA, Radio Free Europe/Radio Liberty, aliachiliwa kutoka Belarus Jumatano baada ya kufungwa jela kwa zaidi ya miaka mitatu. Kesi yake ilionwa na wengi kama iliyochochewa kisiasa.
Pandisha zaidi