Huku shinikizo la kimataifa likiongezeka kwa Rwanda kuzuia mapigano mashariki mwa DRC, mzozo huo ulitarajiwa kugubika mkutano uliofunguliwa mjini Addis Ababa.
Rais wa Rwanda, Paul Kagame, alionekana akihudhuria mikutano katika mkutano huo, lakini rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Felix Tshisekedi, hakuwepo katika mkutano huo wakati waasi wa M23 wakisonga mbele katika ardhi ya nchi yake.
Baada ya kulitimua jeshi la Congo na kuteka Goma, Kivu Kaskazini mwezi uliopita, waasi wanaoungwa mkono na Rwanda walisonga kwenda Kivu Kusini.
Forum