Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatano, Aprili 02, 2025 Local time: 16:05

Hamas yaachia mateka zaidi wa Israel


Hamas imewaachilia huru mateka wengine watatu Jumamosi kwa mabadilishano na wafungwa wa Kipalestina huku sitisho tete la mapigano likitekelezwa licha ya mivutano wa karibuni.

Mmarekani mwenye asili ya Israel Sagui Dekel Chen, 36, mkazi wa Kibbutz Nir Oz kusini mwa Israel, aliripotiwa kuchukuliwa mateka alipokabiliana na wanamgambo wa Hamas wakati wa shambulizi la kigaidi la Oktoba 7, 2023 kusini mwa Israel.

Miezi miwili baada ya kukamatwa kwake, mkewe, Avital, alijifungua binti yao wa tatu. Aliyetolewa pia alikuwa Mrussia mwenye asili ya Israel, Sasha Troufanov, 29, pia kutoka Kibbutz Nir Oz.

Alichukuliwa wakati wa shambulizi la Hamas, pamoja na mama yake, Yelena, Bibi yake Irina Tati, na mwenza wake Sapir Cohen.

Wanawake wote watatu waliachiliwa kwa makubaliano ya mateka mwezi mmoja baadaye. Baba yake, Vitaly, aliuwawa katika shambulizi hilo. Familia ilihamia Israeli kutoka Russia, miaka 25 iliyopita.

Forum

XS
SM
MD
LG