Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatano, Aprili 02, 2025 Local time: 22:56

Miili 50 yapatikana kwenye makuburi ya watu wengi nchini Libya


Wafanyakazi wa wizara ya sheria wakichimba eneo linalodhaniwa kuwa kaburi la watu wengi katika mji wa Tarhouna, Libya. Juni 23, 2020. Picha ya AP
Wafanyakazi wa wizara ya sheria wakichimba eneo linalodhaniwa kuwa kaburi la watu wengi katika mji wa Tarhouna, Libya. Juni 23, 2020. Picha ya AP

Mamlaka nchini Libya zilipata karibu miili 50 kwenye makaburi mawili ya watu wengi katika jangwa la kusini mashariki mwa nchi hiyo, maafisa walisema Jumapili.

Ni mkasa wa hivi karibuni uliohusisha watu wanaotaka kufika Ulaya kupitia nchi hiyo ya Afrika Kaskazini inayokumbwa na machafuko.

Kaburi la kwanza la watu wengi likiwa na miili 19 liligunduliwa siku ya Ijumaa katika shamba katika mji wa kusini mashariki wa Kufra, idara ya usalama ilisema, na kuongeza kuwa maafisa walichukuwa miili hiyo kwa ajili ya vipimo vya uchunguzi wa maiti.

Maafisa waliweka picha kwenye ukurasa wa Facebook zikionyesha maafisa wa polisi na madaktari wakichimba mchangani na kuopoa maiti zilizokuwa zimefungwa kwenye blanketi.

Shirika moja la hisani The al-Abreen charity, ambalo linasaidia wahamiaji mashariki na kusini mwa Libya, lilisema kuwa baadhi ya watu hao walipigwa risasi na kuuawa kabla ya kuzikwa.

Kaburi tofauti la watu wengi, lenye takriban miili 30, pia liligunduliwa Kufra baada ya uvamizi wa kituo cha usafirishaji haramu wa binadamu, kulingana na Mohamed al-Fadeil, kiongozi wa idara ya usalama huko Kufra.

Manusura walisema karibu watu 70 walizikwa kwenye kaburi hilo, aliongeza.

Forum

XS
SM
MD
LG