Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatano, Aprili 02, 2025 Local time: 23:05

Trump aashiria mpango wa kuondolewa kwa Wapalestina kutoka Gaza


Rais wa Marekani Donald Trump akiwa na Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu kwenye Ikulu ya Marekani. Jumanne Feb 4, 2025.
Rais wa Marekani Donald Trump akiwa na Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu kwenye Ikulu ya Marekani. Jumanne Feb 4, 2025.

Rais wa Marekani Donald Trump ameendelea kusisitiza mpango wake wa kuondolewa kwa Wapalestina kutoka Gaza wakati akiwa mwenyeji wa Waziri Mkuu wa Israel Benjamini Netanyahu huko White House Jumanne.

“Nafikiri wanahitaji kupewa ardhi mpya inayopendeza na tutafute watu kadhaa watakao itengeneza na kuifanya inayoweza kukalika,” Trump aliambia wanahabari kabla ya kushiriki kikao na Netanyahu.

Tangazo hilo lilifuatia pendekezo la kushtukiza la Trump mapema Jumanne la kuhamishwa kwa kudumu kwa Wapalestina kutoka Gaza hadi kwenye nchi jirani.

Akizungumza na wanahabari awali kwenye White House, mjumbe wa Marekani huko Mashariki ya Kati Steve Witkoff aliashiria kuwa utawala wa Trump unatathmini mashauriano zaidi kuhusu mkataba wa sitisho la mapigano uliotangazwa Januari 19, siku moja kabla ya kuapishwa kwa Trump.

Mwezi uliopita, Trump alipendekeza kuwa angependa Jordan na Misri wapokee Wapalestina zaidi kama sehemu ya juhudi za kusafisha Gaza.

Forum

XS
SM
MD
LG