Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatano, Aprili 02, 2025 Local time: 18:23

China kuimarisha ushirikiano na Umoja wa Ulaya


Rais wa China Xi Jinping (kushoto) na mwenzake wa Marekani Donald Trumo
Rais wa China Xi Jinping (kushoto) na mwenzake wa Marekani Donald Trumo

China imesema kwamba ipo tayari kushirikiana na Umoja wa Ulaya kukabiliana na changamoto zinazoukumba ulimwengu.

Wizara ya mambo ya nje ya China imesema hayo wakati Umoja wa Ulaya unajitayarisha na uwezekano wa kuwekewa nyongeza ya ushuru kutoka Marekani.

Msemaji wa wizara ya mambo ya nje ya China Lin Jian, amesema kwamba China inatambua umuhimu mkubwa wa ushirikiano na Umoja wa Ulaya na kwamba ina matumaini ushirikiano huo utakuwa wa kutegemewa.

Mkuu wa biashara wa Umoja wa Ulaya amesema kwamba umoja huo unataka kujadiliana kwa haraka sana na Marekani kuhusu mpango wa Donald Trump kuiwekea vikwazo.

Rais wa tume ya Umoja wa Ulaya Ursula Von der Leyen ametabiri kwamba mazungumzo na Washington yatakuwa magumu.

Forum

XS
SM
MD
LG