Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatano, Aprili 02, 2025 Local time: 22:18

Takriban watu 70 wauwawa kwenye mapigano ya Puntland, Somalia


Vikosi vya Puntland vikionyesha wanajeshi wapya waliyopata mafunzo kwenye picha ya Jan. 30, 2025.
Vikosi vya Puntland vikionyesha wanajeshi wapya waliyopata mafunzo kwenye picha ya Jan. 30, 2025.

Karibu watu 70 wameuwawa na wengine 50 kujeruhiwa kufuatia mapigano ya saa 24 kati ya wapiganaji wa Islamic State na vikosi vya eneo la Somalia la Puntland.

Takriban wanajeshi 15 wa Puntland na zaidi ya wanamgambo 50 walikufa kwenye mapigano hayo kwenye maeneo ya Dharin na Qurac kwenye milima ya Cal Miskaad huko Bari Puntland. Taarifa hizo zimetolewa na maafisa kadhaa wa usalama wa Puntland wakizungumza na VOA kwa masharti ya kutotambulishwa kwa kuwa hawajaruhusiwa kuongea na vyombo vya habari.

Kwenye mahojiano ya Jumatano na VOA Idhaa ya Kisomali, msemaji wa operesheni ya usalama wa Puntland Brigedia Jenerali Mohamud Ahmed alisema kuwa mapigano hayo yaliyoanza Jumanne yalikuwa mabaya zaidi tangu Puntland ilipoanza mashambulizi mwezi uliyopita dhidi wanamgambo wa Islamic State ambao wana mahandaki kwenye sehemu za milima.

“Tumedhibitisha kuwa takriban wanamgambo 57 wa Islamic State wote wakiwa raia wa kigeni waliuwawa kwenye mapigano katika saa 24 zilizopita,” Ahmed alisema. Hata hivyo Ahmed hakusema ni wanajeshi wangapi wa Puntland waliuwawa au kujeruhiwa ingawa aliashiria kuwa idadi ilikuwa kubwa.

Forum

XS
SM
MD
LG