Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatatu, Machi 31, 2025 Local time: 07:55

Wanajeshi wa Israel kuendelea kubaki Ukingo wa Magharibi


Waziri wa ulinzi wa Israel, Jumapili amesema wanajeshi wataendelea kubaki katika sehemu za Ukingo wa Magharibi unaokaliwa na walozwezi ambapo Israel imefanya mashambulizi ya wiki nzima, huku ikisema inazidisha uchunguzi wake katika eneo la Palestina.

Israel ilifanya mashambulizi makubwa kaskazini mwa Ukingo wa Magharibi, Januari 21, siku mbili baada ya kusitisha mapigano ambayo yalisimamisha vita Gaza, na kisha kuyapanua kujumuisha maeneo mengine ya karibu.

Israel inasema imedhamiria kukomesha wanamgambo katika eneo hilo, lakini Wapalestina wanaona uvamizi huo kama sehemu ya juhudi za kuimarisha udhibiti wa Israel katika eneo hilo, ambapo Wapalestina milioni 3 wanaishi chini ya utawala wa kijeshi.

Uvamizi huo umekuwa mbaya na kusababisha uharibifu kwa maeneo ya mijini na maelfu ya watu kuyahama makazi yao.

Forum

XS
SM
MD
LG