Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatatu, Machi 31, 2025 Local time: 05:27

Uchaguzi wa Ujerumani wafanyika Jumapili


Wapiga kura wa Ujerumani wanachagua serikali mpya katika uchaguzi wa Jumapili uliotawaliwa na wasiwasi kuhusu kudorora kwa miaka mingi kwa uchumi mkubwa zaidi wa Ulaya, shinikizo la kuzuia uhamiaji na kutokuwa na uhakika juu ya mustakabali wa Ukraine na muungano wa Ulaya na Marekani.

Upinzani wa mrengo wa kati unatarajiwa kushinda, wakati kura za maoni zinaonyesha matokeo mazuri zaidi kwa chama cha mrengo wa kulia toka vita vya pili vya Dunia.

Ujerumani ndiyo nchi yenye watu wengi zaidi katika Umoja wa Ulaya wenye nchi 27 na mwanachama mkuu wa NATO. Imekuwa muuzaji mkubwa wa pili wa silaha kwa Ukraine, baada ya Marekani.

Itakuwa muhimu katika kushughulikia mwitikio wa changamoyo za bara hilo kwa miaka ijayo, ikiwa pamoja na sera ya makabiliano ya serikali ya Trump katika sera za nje na biashara.

Wagombea wakuu ni Mhafidhina Friedrich Merz na Kansela wa sasa Olaf Scholz wa Social Democrats.

Forum

XS
SM
MD
LG