Mamia ya waandamanaji walishika mabango yaliyoandikwa “Asante Mungu kwa ajili ya Rais Trump” na kuonyesha ujumbe mwingine wa kukosoa kile wanachokiona kuwa sheria za kibaguzi zilizoanzishwa na serikali ya Afrika Kusini zinazowabagua wazungu walio wachache.
Wengi wanatoka jumuiya ya Afrikana ambayo Trump alizingatia katika amri ya utendaji wiki moja iliyopita ambapo alipunguza misaada na usaidizi kwa serikali ya Afrika Kusini inayoongozwa na Weusi.
Katika agizo hilo, Rais Trump amesema Waafrika Kusini, ambao ni walowezi wa kikoloni wa Uholanzi, wanalengwa na sheria mpya inayoruhusu serikali kuchukua ardhi binafsi.
Afrika Kusini imekanusha madai ya Rais Trump.
Forum