Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatano, Aprili 02, 2025 Local time: 17:57

Russia yaongeza kasi ya mashambulizi Ukraine


Wanajeshi wa Russia, wameongeza kasi ya mashambulizi yao mashariki mwa Ukraine, jeshi la Kyiv, limesema Jumapili, huku afisa wa NATO akitabiri kuwa Moscow itaongeza kasi na nguvu ya mashambulizi yake wakati mazungumzo ya kumaliza vita yanakaribia.

Mashambulizi makubwa yalifanyika karibu na kituo cha vifaa kilicho hatarini cha Pokrovsk, Kyiv imesema, huku maafisa wa Marekani na Russia, wakitarajiwa kufanya mazungumzo katika siku zijazo nchini Saudi Arabia na Rais wa Marekani, Donald Trump akishinikiza amani.

Jeshi la Kyiv limeripoti mapigano 261 na Russia, katika saa 24 siku ya Jumamosi, ikiwa ni idadi kubwa zaidi iliyorekodiwa mwaka huu na zaidi ya mara mbili ya takriban 100 kwa siku kuliko ilivyoripotiwa siku zilizopita.

β€œLeo ilikuwa siku ngumu zaidi ya 2025 kwenye uwanja wa mapambano,” blogu ya kijeshi ya Ukraine, ya DeepState iliandika Jumamosi jioni.

Forum

​
XS
SM
MD
LG