Hati ya kumkamata Yoon kwa misingi ya kufanya uasi inatarajiwa muda wake kumalizika usiku wa manane siku ya Jumatatu.
Wadhifa wa Sarkozy umegubikwa na matatizo ya kisheria tangu aliposhindwa uchaguzi wa rais mwaka 2012.
Wapigana wa Wagner wamekuwepo nchini Mali tangu jeshi lilipokamata madaraka katika mapinduzi ya mwaka 2020 na 2021
Meloni alionekana mshirika mwenye nguvu kwa Trump kutokana na yeye kuwa M-conservative na mrengo wa kulia huko Italy.
Mwanadiplomasia wa Syria na afisa wa Qatar wameithibitisha AFP imefanya mkutano na waziri wa muda wa mambo ya nje wa Syria
Serikali ya kijeshi ya Myanmar imewaachia huru zaidi ya wafungwa 6,000 na kupunguza adhabu za vifungo vya wafungwa wengine, kama sehemu ya msamaha kwa watu wengi katika kuadhimisha miaka 77 ya uhuru wake kutoka kwa Uingereza siku ya Jumamosi.
Kansela wa Ujerumani Olaf Scholz katika mahojiano yaliyochapishwa Jumamosi , amelaani matamshi “ ya ovyo ” ya Elon Musk na msimamo wake wa wazi kukiunga mkono chama cha mrengo mkali wa kulia cha AfD.
Wizara ya ulinzi ya Russia Jumamosi imesema wanajeshi wa Russia wamedhibiti kijiji cha Nadiya katika mkoa wa mashariki mwa Ukraine wa Luhansk na kutungua makombora manane yaliyotengezwa Marekani aina ya ATACMS.
Wizara ya afya ya Palestina katika Ukingo wa Magharibi unaokaliwa kimabavu imesema mtu mmoja aliuawa na wengine tisa kujeruhiwa katika shambulio la Israel kwenye kambi ya wakimbizi, huku jeshi la Israel likisema Jumamosi kwamba limewafyatulia risasi “magaidi.”
Watu wenye silaha kutoka Nigeria wamewaua wanajeshi watano wa Cameroon na kuwajeruhi wengine kadhaa katika kijiji cha Bakinjaw kwenye mpaka wa Cameroon na Nigeria, mbunge wa wilaya alisema Jumamosi.
Rais wa Ghana anayeondoka madarakani Nana Akufo Addo Ijumaa ametangaza kuwa watu wote wenye passpoti za Afrika kuanzia mwaka huu wataingia nchini humo bila ya visa, hatua inayoashiria kuelekea muingiliano wa kiuchumi barani Afrika.
Pandisha zaidi