Zaidi ya wakimbizi wa ndani 55,000 wa Sudan wamerejea katika maeneo ya kusini mashariki mwa jimbo la Sennar, zaidi ya mwezi mmoja baada ya jeshi kutwaa tena mji mkuu wa jimbo hilo kutoka kwa wanamgambo, shirika la Umoja wa Mataifa la uhamiaji limesema Jumamosi.
Rais wa Korea Kusini, aliyeondolewa madarakani Yoon Suk Yeol alifikishwa mahakamani kwa mara ya kwanza Jumamosi kwa ajili ya kusikilizwa kwa kesi muhimu ambayo itaamua kuhusu kuongeza muda wake wa kuzuiliwa huku wapelelezi wakichunguza maombi yake ya sheria ya kijeshi yaliyo shindikana.
Baraza la Mawaziri la Israel, Jumamosi limeidhinisha makubaliano ya kusitisha mapigano ya Gaza na kuachiliwa kwa mateka ambayo yatasimamisha vita vya miezi 15 na Hamas.
Serekali ya Sydney Jumamosi imetangaza janga la asili katika sehemu za mashariki mwa Australia ambako upepo umeangusha miti na kukata umeme kwa maelfu ya nyumba.
Rais wa Colombia, Gustavo Petro, Ijumaa amesema kwamba anasitisha mashauriano ya amani na wanamgambo wa National Liberation Army (ELN) siku moja baada ya ghasia kati ya makundi yenye silaha kaskazini mashariki na kusababisha vifo vya takriban watu 30.
Wizara ya fedha ya Marekani Alhamisi ilitangaza vikwazo dhidi ya Abdel Fattah al-Burhan, ikilituhumu jeshi lake kwa kushambulia shule masoko na hospitali pamoja na kutumia mtindo wa kuwanyima wananchi chakula kama silaha.
Idadi kubwa ya wabunge wanamkata Biden kutoa afueni ili kuzuia mtandao wa TikTok kufungwa nchini Marekani ifikapo Jumapili, na kuonya kuwa mamilioni ya wabunifu na biashara zinaweza kuathiriwa.
Uingereza na Ukraine Alhamisi zilisaini makubaliano ya miaka 100, huku Uingereza ikiahidi kuipa Ukraine msaada wa kijeshi wa dola bilioni 3.6 mwaka huu.
Takriban wanahabari 67 wanafungwa jela barani kote Afrika, hali hiyo ikiashiria changamoto inayoendelea ya kuwa na vyombo vya habari huru, kulingana na ripoti iliyotolewa Alhamisi.
Marekani imemuwekea vikwazo kiongozi wa jeshi la Sudan, ikitaja kuhusika kwake katika uhalifu wa kivita katika mzozo ambao umelitumbukiza taifa hilo lenye utajiri wa mafuta katika hali mbaya tangu mwaka jana, kusababisha njaa, kuua maelfu ya watu na kuwakosesha makazi mamilioni ya wengine.
Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu alisema Alhamisi kwamba mgogoro wa dakika za mwisho na Hamas unazuia idhini ya Israeli ya makubaliano yaliyosubiriwa kwa muda mrefu ya kusitisha mapigano katika Ukanda wa Gaza na kuwaachilia mateka kadhaa.
Waokoaji wa Afrika Kusini walikuwa wakifanya juhudi za mwisho siku ya Alhamisi kufahamu kama kuna mtu yeyote aliyenusurika kwenye machimbo haramu ya dhahabu
Pandisha zaidi