Rais wa Ghana anayeondoka madarakani Nana Akufo Addo Ijumaa ametangaza kuwa watu wote wenye passpoti za Afrika kuanzia mwaka huu wataingia nchini humo bila ya visa, hatua inayoashiria kuelekea muingiliano wa kiuchumi barani Afrika.
Waziri mkuu wa Thailand Paetongtarn Shinawatra Ijumaa alitangaza mali zenye thamani ya zaidi ya dola milioni 400, chama chake kimesema, ikijumuisha zaidi ya mikoba ya mkononi 200 iliyotengenezwa na wabunifu yenye thamani ya dola milioni 2 na saa 75 za kifahari zenye thamani ya dola milioni 5.
Mamlaka za Korea Kusini Ijumaa zimesimamisha jaribio la kumkamata Rais aliyeondolewa baada ya kushtakiwa na bunge Yoon Suk Yeol kufuatia hali ya mvutano mkali wa saa sita kati ya wachunguzi na maafisa wa usalama watiifu kwa rais huyo.
Jeshi la Israel limeripoti kwamba limetungua kombora na ndege isiyokuwa na rubani iliyorushwa Ijumaa kutoka Yemen, ukiwa msururu wa mashambulizi ya hivi karibuni kutoka nchini humo kuilenga Israel katika wiki za hivi karibuni.
Wahamiaji 27 wakiwemo wanawake na watoto, walifariki wakati boti mbili zilipopinduka kwenye pwani katikati mwa Tunisia, huku watu 83 waliokolewa, afisa wa ulinzi wa kiraia aliliambia shirika la habari la AFP siku ya Alhamisi.
Waandamanaji kadhaa walikusanyika katika mji wa Douma nchini Syria, Jumatano kudai majibu katika kutoweka kwa wanaharakati wanne mashuhuri waliotekwa nyara zaidi ya muongo mmoja uliopita.
Dereva mmoja aliendesha gari kwenye umati wa watu waliokuwa wakisherehekea Mwaka Mpya, Jumatano mapema mjini New Orleans na kufyatua risasi, na kuuwa watu 10 pamoja na kujeruhi wengine zaidi ya 35 katika shambulizi FBI imesema inachunguza kama kitendo cha kigaidi.
Rais Joe Biden wa Marekani ametoa maelezo mafupi kuhusiana na tukio na mauajai na majeruhi la New Orleans kabla ya kuondoka Wilmington, Delaware.
Rais wa Ivory Coast Alassane Ouattara alisema katika hotuba yake ya mwisho wa mwaka kwamba wanajeshi wa Ufaransa wataondoka katika taifa hilo la Afrika Magharibi mwezi huu wa Januari.
Maafisa wa Palestina wamesema mashambulizi ya anga ya Israel kaskazini na kati kati mwa Gaza yamesababisha vifo vya watu 15.
Rais wa Ivory Coast Alassane Ouattara katika hotuba yake ya mwisho wa mwaka anataka wanajeshi wa Ufaransa kuondoka katika taifa hilo la Afrika Magharibi kuanzia mwezi wa kwanza.
Watu kumi waliuawa na 35 kujeruhiwa baada ya mshukiwa kuvurumisha gari lake kwenye umati wa watembea kwa miguu katika Barabara yenye shughuli nyingi ya French Quarter huko New Orleans leo saa tisa na robo alfajiri siku ya Jumatano kwenye mtaa wa Bourbon.
Pandisha zaidi