Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu alisema Alhamisi kwamba mgogoro wa dakika za mwisho na Hamas unazuia idhini ya Israeli ya makubaliano yaliyosubiriwa kwa muda mrefu ya kusitisha mapigano katika Ukanda wa Gaza na kuwaachilia mateka kadhaa.
Waokoaji wa Afrika Kusini walikuwa wakifanya juhudi za mwisho siku ya Alhamisi kufahamu kama kuna mtu yeyote aliyenusurika kwenye machimbo haramu ya dhahabu
Huku muda wa mwisho wa Jumapili ukikaribia kwa Tiktok kutafuta mmiliki mwingine au kukabiliwa na vikwazo vya Marekani, maelfu ya Wamarekani wanaotumia mtandao huo maarufu wa kijamii wanasema wanahamia kwenye program nyingine ya mtandao wa kijamii wa China, Xiaohongshu au RedNote.
Cuba Jumatano ilianza kuwaachia huru wafungwa waliowekwa jela kufuatia maandamano ya kuipinga serikali ya mwaka 2021, kutokana na makubaliano iliyofikia na utawala wa Biden wiki hii.
Rwanda Jumatano ilibadili kauli kufuatia madai yake ya awali kwamba iligundua akiba yake ya kwanza ya mafuta katika Ziwa Kivu, ikisema bado iko kwenye awamu ya uchunguzi na inatafuta washirika.
Israel na Hamas wamefikia makubaliano ya kusitisha mapigano katika awamu kadhaa ambayo yatapelekea kuachiliwa kwa baadhi ya mateka wanaoshikiliwa na kundi hilo la wanamgambo kwa zaidi ya mwaka mmoja.
Wapalestina wana sherehekea makubaliano ya kusitisha mapigano ya Gaza kati ya Israel na Hamas huku WaIsrael wakiwa bado na wasi wasi kuhusu mateka walobaki.
White House inasema imekamilisha kuweka sheria za kukabiliana na teknolojia ya magari kutoka China na Russia ambazo zitapiga marufuku magari yote yanayotumia umeme kutoka nchi hizo mbili kuingia kwenye soko la Marekani.
Maafisa wa Korea Kusini Jumatano walimkamata Rais aliyeondolewa na bunge Yoon Suk Yeol kufuatia tuhuma za uasi, huku kiongozi huyo akisema amekubali uchunguzi dhidi yake uendelee ili kuepusha “umwagaji damu”.
Shirika la afya duniani WHO Jumanne limesema kwamba mlipuko unaoshukiwa wa ugonjwa hatari wa Marburg nchini Tanzania umewaua watu wanane, na kuonya kwamba hatari ya kusambaa kwa ugonjwa huo nchini humo ni “kubwa”.
IOM inasema watu waliokoseshwa makaazi Haiti wameongezeka kufikia asilimia 87 kutokana na vurugu za makundi ya uhalifu.
Maafisa wa Ujerumani wamesema ziara hiyo inaihakikishia Ukraine kupata msaada katika vita vyake dhidi ya Russia
Pandisha zaidi