White House inasema imekamilisha kuweka sheria za kukabiliana na teknolojia ya magari kutoka China na Russia ambazo zitapiga marufuku magari yote yanayotumia umeme kutoka nchi hizo mbili kuingia kwenye soko la Marekani.
Maafisa wa Korea Kusini Jumatano walimkamata Rais aliyeondolewa na bunge Yoon Suk Yeol kufuatia tuhuma za uasi, huku kiongozi huyo akisema amekubali uchunguzi dhidi yake uendelee ili kuepusha “umwagaji damu”.
Shirika la afya duniani WHO Jumanne limesema kwamba mlipuko unaoshukiwa wa ugonjwa hatari wa Marburg nchini Tanzania umewaua watu wanane, na kuonya kwamba hatari ya kusambaa kwa ugonjwa huo nchini humo ni “kubwa”.
IOM inasema watu waliokoseshwa makaazi Haiti wameongezeka kufikia asilimia 87 kutokana na vurugu za makundi ya uhalifu.
Maafisa wa Ujerumani wamesema ziara hiyo inaihakikishia Ukraine kupata msaada katika vita vyake dhidi ya Russia
Mazungumzo hayo yanakuja baada ya miezi 15 ya mapigano huko Gaza na yanaelezewa kuleta mafanikio kwa wiki hii.
Rais Joe Biden anayekamilisha muhula wake Jumatatu alipongeza rekodi yake ya sera ya kigeni akisema wapinzani wa Marekani wamekuwa wadhaifu kuliko kipindi alipoingia madarakani miaka minne iliyopita, licha ya mizozo ya kimataifa ambayo bado haijatatuliwa.
Kiongozi wa upinzani nchini Comoros Jumatatu alitupilia mbali matokeo ya uchaguzi wa wabunge, ambao ulisusiwa kwa kiasi kikubwa na wapinzani, kwa madai ya “udanganyifu mkubwa”.
Maafisa wa usalama nchini Somalia wamesema waliwauwa wapiganaji kadhaa wa kundi la Islamic State na kuteka vituo vinane vya wanajihadi wakati wa operesheni ya kijeshi inayoendelea katika jimbo huru la Puntland.
Watu 100 ambao walikuwa wakichimba madini kinyume cha sheria katika mgodi wa dhahabu usiofanya kazi nchini Afrika Kusini walifariki baada ya kunaswa chini ya mgodi huo kwa miezi kadhaa, huku polisi wakijaribu kuwaondoa huko, kundi linalowakilisha wachimba migodi hao lilisema Jumatatu.
Bunge jipya la Msumbiji limekutana Jumatatu kwenye mji mkuu , ambapo wabunge 210 walikula viapo vyao huku vyama vya upinzani vikisusia na kuendelea na maandamano baada ya kupinga matokeo ya uchaguzi mkuu uliomalizika hivi karibuni.
Mwanahabari na mwanaharakati Maria Sarungi hatimaye amevunja ukimya kufuatia jaribio la kumteka nyara siku ya jumapili Nairobi, Kenya
Pandisha zaidi