Miongoni mwa amri za kiutendaji zililenga uhamiaji kama vile kutangaza hali ya dharura kwenye mpaka wa Marekani na Mexico.
Rubio ameanza kazi akiwa mwenyeji wa mkutano na wenzake kutoka Australia, India na Japan.
Vizuizi haviongozi mahala popote na hakuna mshindi katika vita vya kibiashara, anasema Makamu wa Waziri Mkuu wa China, Ding
Akizungumza baada ya kula kiapo kama rais wa 47 wa Marekani siku ya Jumatatu Januari 20, 2025, ndani ya ukumbi wa Rutanda katika jengo la bunge, Rais Trump amesema ataleta mapinduzi katika maisha ya Wamarekani.
Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan Jumatatu alithibitisha uwepo wa mlipuko hatari wa virusi vya Marburg kaskazini magharibi mwa nchi, huku kesi nyingine moja ya ugonjwa huo ikiripotiwa.
Viongozi mbali mbali wa mataifa Jumatatu wameendelea kumpongeza rais mpya wa Marekani Donald Trump, kufuatia kuapishwa kwake kama rais wa 47.
Rais mpya wa Marekani Donald Trump Jumatatu usiku baada yakuapishwa mchana alikutana na maelfu ya wafuasi wake kwenye ukumbi wa Capitol One Arena mjini Washington DC.
Donald Trump ameapishwa leo Jumatatu kuchukua rasmi hatamu za uongozi kama rais wa 47 wa Marekani. Kurejea kwake madarakani ni tukio la kihistoria kwa mtu ambaye katika kipindi cha zaidi ya miaka tisa alikibadili chama cha Republican katika nchi inayozidi kukumbwa na migawanyiko.
Rais mteule wa Marekani Donald Trump Jumapili amewahutubia maelfu ya wafuasi wake kwenye jiji kuu la Marekani Washington akiwaahidi kuchukua hatua kali dhidi ya uhamiaji.
Rais mteule Donald Trump, Jumapili amesema anapanga kutoa amri ya kiutendaji ambayo itaipatia kampuni mama ya mtandao wa TikTok, yenye makao yake China muda zaidi wa kutafuta mnunuzi aliyeidhinishwa kabla ya mtandao huo maarufu wa video kukabiliwa na marufuku ya kudumu ya Marekani.
Rais wa Marekani, Joe Biden, Jumapili amemsamehe mzalendo mweusi Marcus Garvey, ambaye alimshawishi Malcolm X na viongozi wengine wa haki za kiraia ambaye alipatikana na hatia ya ulaghai wa barua katika miaka ya 1920.
Usitishaji mapigano uliokuwa ukitarajiwa kati ya Israel na Hamas umeanza baada ya kucheleweshwa kwa karibu saa tatu wakati Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu, aliposema kuwa hautaanza isipokuwa Hamas itatoa orodha ya mateka watatu waliopangwa kuachiliwa Jumapili.
Pandisha zaidi