Waziri wa ulinzi wa Marekani Lloyd Austin Jumanne amethibitisha tena kile alichokiita uungwaji mkono usiotetereka wa ulinzi kwa Japan na Korea Kusini katika kukabiliana na changamoto zinazosababishwa na China katika eneo la East China Sea.
Waziri mkuu wa israel Benjamin Netanyahu amefika katika mahakama ya Tel Aviv Jumanne kwa mara ya kwanza katika kesi ya rushwa inayomkabili kwa muda mrefu.
Familia za wafungwa wa Syria Jumatatu zilikuwa zinazunguka kwenye vyumba vichafu katika jela ya Sednaya mjini Damascus kujaribu kuona dalili za kuwpata jamaa zao waliofungwa kwa muda mrefu pale milango ilipofunguliwa na waasi.
Kiongozi wa waasi nchini Syria Abu Mohammed al-Golani kwa mara ya kwanza Jumatatu amekutana na waziri mkuu anayeondoka madarakani kufuatia kusonga mbele kwa haraka kwa waasi ambao walimuondoa rais Bashar al Assad.
Ripoti mbalimbali nchini Tanzania zinaonyesha rushwa kubaki kuwa changamoto kubwa inayoathiri sekta nyingi nchini, huku vijana wakiathirika zaidi.
WHO ilisema kesi 406 za ugonjwa huo usiojulikana zilirekodiwa Oktoba 24 hadi Disemba 5 ambapo wagonjwa 31 walifariki.
Rais wa Marekani Joe Biden Jumapili amesema kuwa kuanguka ghafla kwa serikali ya Syria ya Bashar al Assad ni “kitendo cha msingi cha haki,” lakini ni wakati wa kutokuwa na uhakika kwa Mashariki ya Kati.
Rais-mteule wa Marekani, Donald Trump ameapa kufanya mabadiliko makubwa na ya haraka baada ya kuchukua ofisi Januari 20, kwa kuwarudisha makwao mamilioni ya wahamiaji walio ndani ya nchi kinyume cha sheria.
Rais mteule wa Marekani Donald Trump Jumapili ametoa wito wa sitisho la haraka la mapigano na mazungumzo kati ya Ukraine na Russia ili kumaliza “vita visivyo na maana”, na kupelekea Rais Volodomyr Zelenskiy kusema amani haiwezi kupatikana bila dhamana.
Vyanzo ndani ya makundi ya wanamgambo wa Palestina huko Gaza Jumapili vimesema kwamba Hamas imewataka kukusanya taarifa kuhusu mateka wanaoshikiliwa na makundi hayo kwa ajili ya maandalizi ya makubaliano ya kusitisha mapigano na kuwaachilia mateka na Israel.
Mtandao wa kundi la waokoaji wa kujitolea nchini Sudan umesema raia 28 wameuawa Jumapili wakati kituo cha mafuta kilichopo katika eneo la Khartoum chini ya udhibiti wa kundi la RSF kiliposhambuliwa kwa makombora.
Pandisha zaidi