Wanajeshi wa Marekani wameanza kuondoka kidogo kidogo kutoka Okinawa hadi Guam, miaka 12 baada ya Japan na Marekani kukubaliana kuhusu marekebisho yao ili kupunguza mzigo mkubwa wa kuwepo kwa wanajeshi wa Marekani katika kisiwa cha kusini mwa Japan.
Vifaru wanne weupe wamekufa nchini Zimbabwe baada ya kunywa maji kutoka katika ziwa lililochafuliwa na maji taka ambalo pia ndilo msambazaji mkuu wa maji karibu na mji mkuu
Mazungumzo ya Umoja wa Mataifa yanayosimamiwa na Saudi Arabia yalishindwa kufikia makubaliano ya jinsi ya kukabiliana na ukame
Mchezaji soka wa zamani Mikheil Kave-lashvili amechaguliwa kuwa rais wa Georgia
Bunge la Korea Kusini limepiga kura kumshtaki kutaka kumuondoa madarakani Rais Yoon Suk Yeol kwa tangazo lake la muda mfupi la sheria ya kijeshi mwezi huu.
Rais mteule wa Ghana John Dramani Mahama amesema hataachana na mpango wa dola bilioni 3 wa kuokoa uchumi wa nchi hiyo na Shirika la Kimataifa la Fedha -IMF,
Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron Ijumaa amemteua waziri mkuu mpya Francois Bayrou, kiongozi wa chama cha mrengo wa kati baada ya mazungumzo magumu ili kumpata mrithi wa Michel Barnier aliyeondolewa na bunge wiki iliyopita, Ikulu ya Ufaransa imetangaza.
Niger Alhamisi ilitangaza kwamba imesitisha matangazo ya radio BBC kwa miezi mitatu, huku shirika hilo la utangazaji la Uingereza likiingia kwenye orodha ya vyombo vya habari vya nchi za Magharibi vilivyoadhibiwa na serikali za kijeshi katika kanda ya Sahel.
Umoja wa Mataifa Jumatano umeonya kuwa uamuzi wa Taliban wa kuwazuia wanawake kusomea utabibu kutaharibu hali zaidi Afghansitan ambayo tayari inakabiliwa na janga baya sana la kibinadamu.
Uungaji mkono wa vyama vya mrengo wa kulia barani Ulaya umeendelea kukua mwaka huu licha ya wasi wasi wa wapiga kura kuhusu uhamiaji, mfumuko wa bei na vita nchini Ukraine.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres, Alhamisi ameziomba nchi tajiri kutimiza ahadi zao ya kuzisaidia nchi masikini katika kukabiliana na mabadiliko ya hali ya hewa.
Rais wa Marekani Joe Biden Jumatano amesema kuwa anajivunia kuona kwamba program ya utafiti wa afya ya wanawake aliyoianzisha mwaka jana kupitia ushawishi wa mke wake, tayari imewekeza karibu dola bilioni moja, kwa kuwa afya njema kwa wanawake inaimarisha ustawi wa Marekani.
Pandisha zaidi