Mtaalam wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa nchini Haiti, William O’Neil Jumanne ameambia wanahabari mjini New York kwamba hali ya kiusalama nchini humo ni tete huku akisihi wahusika wa kitaifa na kimataifa kuheshimu haki za binadamu.
Maafisa wa Ufilipino wanasema Rais wa zamani wa nchi hiyo aliyekamatwa Rodrigo Duterte aliondoka mjini Manila akiwa ndani ya ndege na atakabidhiwa Mahakama ya Kimataifa ya Jinai mjini The Hague.
Angola Jumanne ilisema itajaribu kuanzisha katika siku zijazo mazungumzo ya moja kwa moja kati ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na waasi wa M23 ambao inasemekana wanaoungwa mkono na Rwanda.
Rais wa Marekani Donald Trump Jumanne alasiri alibadili msimamo kuhusu tishio lake la kuongeza maradufu ushuru kwenye chuma na aluminum kutoka Canada.
Maafisa wa Marekani na Ukraine walikutana Jumanne mjini Jeddah, Saudi Arabia kwa mazungumzo kuhusu juhudi za kumaliza vita kati ya Russia na Ukraine, huku pande zote mbili zikisema Kyiv inaunga mkono mpango wa Marekani wa sitisho la mapigano kwa siku 30.
Basi hilo lilibeba zaidi ya watu 50 waliokuwa wanakwenda kazini wakati lilipoanguka katika barabara yenye shughuli nyingi.
Mivutano kati ya Rais Salva Kiir na Makamu wake wa Kwanza wa Rais Riek Machar ikizusha hofu ya kurejea vita vya wenyewe kwa wenyewe.
Kundi la Al Shabaab limedai kuhusika na shambulio hilo katika taarifa yake na lilisema limewaua zaidi ya watu 10.
Serikali kuu ya Syria imefikia makubaliano na mamlaka inayoongozwa na Wakurdi ambao wanadhibiti eneo la kaskazini mashariki mwa nchi, ikiwa ni pamoja na sitisho la mapigano na kushirikishwa katika jeshi la Syria kwa kundi hilo linaloungwa mkono na Marekani.
Tanzania imeripoti visa vya kwanza vya ugonjwa wa Mpox, wizara ya afya ilisema Jumatatu, ikiwa ni mara ya kwanza virusi hivyo kugunduliwa katika mlipuko uliokumba nchi kadhaa za Afrika.
Waziri wa mambo ya nje wa Marekani Marco Rubio Jumatatu alisema Marekani inatumai kutatua suala la misaada kwa Ukraine iliyositishwa katika mazungumzo ya Jumanne na maafisa wa Ukraine mjini Jeddah, Saudi Arabia.
Pandisha zaidi