Basi hilo lilibeba zaidi ya watu 50 waliokuwa wanakwenda kazini wakati lilipoanguka katika barabara yenye shughuli nyingi.
Mivutano kati ya Rais Salva Kiir na Makamu wake wa Kwanza wa Rais Riek Machar ikizusha hofu ya kurejea vita vya wenyewe kwa wenyewe.
Kundi la Al Shabaab limedai kuhusika na shambulio hilo katika taarifa yake na lilisema limewaua zaidi ya watu 10.
Serikali kuu ya Syria imefikia makubaliano na mamlaka inayoongozwa na Wakurdi ambao wanadhibiti eneo la kaskazini mashariki mwa nchi, ikiwa ni pamoja na sitisho la mapigano na kushirikishwa katika jeshi la Syria kwa kundi hilo linaloungwa mkono na Marekani.
Tanzania imeripoti visa vya kwanza vya ugonjwa wa Mpox, wizara ya afya ilisema Jumatatu, ikiwa ni mara ya kwanza virusi hivyo kugunduliwa katika mlipuko uliokumba nchi kadhaa za Afrika.
Waziri wa mambo ya nje wa Marekani Marco Rubio Jumatatu alisema Marekani inatumai kutatua suala la misaada kwa Ukraine iliyositishwa katika mazungumzo ya Jumanne na maafisa wa Ukraine mjini Jeddah, Saudi Arabia.
Sumy iko katika mpaka kutoka mkoa wa Kursk nchini Russia ambako vikosi vya Ukraine vilianzisha mashambulizi mwezi Agosti.
Wakati huo huo Rais wa Taiwan Lai Ching-te amesema ni watu wa Taiwan pekee wanaoweza kuamua mustakabali wao.
Papa Francis alifuatilia ufunguzi wa mkutano huo kwa njia ya video siku ya Jumapili.
Tukio limetokea saa chache baada ya wanajeshi wa Korea Kusini na Marekani kuanza mazoezi yao ya pamoja ya kila mwaka.
Kiongozi wa Kanisa Katoliki duniani Papa Francis, ambaye afya yake imeendelea kuimarika wakati akipokea matibabu kutokana na homa ya mapafu, Jumapili aliwashukuru madaktari pamoja na wahudumu wa afya, ingawa hakuweza kuongoza maombi ya Angelus kwa mara ya nne mfululizo.
Pandisha zaidi