Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumapili, Machi 30, 2025 Local time: 23:42

Angola kuanzisha mazungumzo kati ya serikali ya DRC na waasi wa M23


Rais wa DRC Felix Tshisekedi na Rais wa Angola Joao Lourenco
Rais wa DRC Felix Tshisekedi na Rais wa Angola Joao Lourenco

Angola Jumanne ilisema itajaribu kuanzisha katika siku zijazo mazungumzo ya moja kwa moja kati ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na waasi wa M23 ambao inasemekana wanaoungwa mkono na Rwanda.

Hapakuwa maelezo ya moja kwa moja kutoka serikali ya Congo, ambayo imekuwa ikipinga mara kwa mara kufanya mazungumzo na M23.

Taifa hilo la kusini mwa Afrika limekuwa likijaribu kuwa mpatanishi ili kufikia sitisho la mapigano la kudumu na kupunguza mvutano kati ya Congo na jirani yake Rwanda, ambayo imekuwa ikituhumiwa kuwaunga mkono M23.

Rwanda inakanusha kutoa silaha na wanajeshi kwa waasi wa M23, na inasema kile jeshi lake inachofanya ni kujihami dhidi ya jeshi la Congo na wanamgambo wenye nia mbaya dhidi ya Kigali.

Waasi wa M23 waliteka miji mikubwa ya mashariki mwa Congo tangu mwezi Januari.

Rais wa DRC Felix Tshisekedi alifanya ziara ya kikazi mjini Luanda na alikutana na mwenzie Joao Lourenco, ofisi ya rais wa Angola ilisema katika taarifa kwenye Facebook.

“Angola kama mpatanishi katika mzozo wa mashariki mwa Congo, itaanzisha mawasiliano na M23, ili wajumbe kutoka Congo na M23 wafanye mazungumzo ya moja kwa moja mjini Luanda katika siku zijazo,” ofisi ya rais iliongeza.

Forum

XS
SM
MD
LG