Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatatu, Machi 31, 2025 Local time: 01:31

Rais wa zamani wa Ufilipino akabidhiwa ICC


Rais wa zamani wa Ufilipino Rodrigo Duterte
Rais wa zamani wa Ufilipino Rodrigo Duterte

Maafisa wa Ufilipino wanasema Rais wa zamani wa nchi hiyo aliyekamatwa Rodrigo Duterte aliondoka mjini Manila akiwa ndani ya ndege na atakabidhiwa Mahakama ya Kimataifa ya Jinai mjini The Hague.

Ndege iliyokuwa inambeba Duterte iliondoka Manila Jumanne jioni. Alikamatwa baada ya kuwasili na familia yake kwenye uwanja wa ndege wa kimataifa wa Manila Jumanne asubuhi akitokea Hong Kong, chini ya hati ya kumkamata ya ICC.

Mahakama hiyo ya kimataifa iliamuru akamatwe baada ya kumshtumu kwa uhalifu dhidi ya ubinadamu kutokana na sera yake mbaya ya kutokomeza biashara ya dawa za kulevya ambayo alikuwa anaisimamia akiwa madarakani, serikali ya Ufilipino imesema.

ICC imekuwa ikifanya uchunguzi wa mauaji makubwa kuhusiana na sera hiyo ya Duterte alipokuwa akihudumu kama meya wa mji wa kusini mwa Ufilipino wa Davao na baadaye kuhudumu kama rais.

Forum

XS
SM
MD
LG