Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumapili, Septemba 08, 2024 Local time: 03:34

Ufaransa yatetea hatua ya kuendelea kuuza silaha Mashariki ya Kati


Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron akiwa na Waziri Mkuu wa Iraq Adel Abdul-Mahdi Paris, Ufaransa, Mei 3, 2019.
Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron akiwa na Waziri Mkuu wa Iraq Adel Abdul-Mahdi Paris, Ufaransa, Mei 3, 2019.

Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron ametetea hatua ya nchi yake kuziuzia silaha Saudi Arabia na umoja wa nchi za kiarabu, huku wanaopinga hatua hiyo wakiangazia shehena mpya ya silaha zinazotarajiwa kuondoka bandari ya Le Havre.

Makundi ya kutetea haki za kibinadamu yameishutumu Ufaransa mara kwa mara kwa kuendelea kutoa silaha kwa mataifa ya Ghuba, licha ya kuwepo madai ya uhalifu wa vita na vifo vya raia wakati wa operesheni za kijeshi nchini Yemen.

Akizungumza na waandishi wa habari alipowasili Romania kwa mkutano wa viongozi wa Umoja wa Ulaya, Macron amesema kwamba silaha zake hazitumiki dhidi ya raia, bali katika vita dhidi ya ugaidi.

Kulingana na mashirika ya kutoa misaada, vita vya Yemen, ambavyo vimedumu kwa muda wa zaidi ya miaka minne, vimeua maelfu ya watu, idadi kubwa wakiwa ni raia.

Imetayarishwa na mwandishi wetu, Washington, DC.

XS
SM
MD
LG