Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Septemba 19, 2024 Local time: 01:14

Sudan: Bwawa lapasuka na kusababisha vifo 30 na kuharibu vijiji 20


Watu wakiwa wamebeba bot katika maji yenye matope baada ya Bwawa la Arbaat kupasuka, of the kilomita 40 kaskazini ya mji wa Port Sudan kufuatia mvua kubwa na mafuriko Agosti 25, 2024.
Watu wakiwa wamebeba bot katika maji yenye matope baada ya Bwawa la Arbaat kupasuka, of the kilomita 40 kaskazini ya mji wa Port Sudan kufuatia mvua kubwa na mafuriko Agosti 25, 2024.

Baadhi ya sehemu za  mashariki mwa Sudan zimekumbwa na mafuriko baada ya bwawa kuvunjika na kuharibu vijiji 20 na kusababisha vifo vya watu 30.

Mvua kubwa zimesababisha mafuriko yaliyojaza bwawa la Arbaat mnamo Jumapili, kilomita 40 kaskazini mwa Port Sudan, mji ambao sasa unatumika kama makao makuu ya serikali, wanadiplomasia, mashirika ya misaada na watu waliokoseshwa makazi kutokana na vita vya miezi kadhaa kati ya jeshi na kikosi cha kijeshi cha RSF.

Umoja wa Mataifa umesema kwamba karibu watu 50,000 wameathiriwa na mafuriko, na kwamba huenda idadi hiyo inajumuisha tu watu waliokuwa wanaishi magharibi mwa bwawa hilo na kwamba si rahisi kuwafikia watu walio mashariki mwa bwawa.

Uharibifu uliotokea katika Bwawa la Arbaat Dam, lilioko kilomita 40 kaskazini mwa Port Sudan lililopasuka kufuatia mvua kubwa na mafuriko Agost 25, 2024. (AFP)
Uharibifu uliotokea katika Bwawa la Arbaat Dam, lilioko kilomita 40 kaskazini mwa Port Sudan lililopasuka kufuatia mvua kubwa na mafuriko Agost 25, 2024. (AFP)

Bwawa hilo lilikuwa chanzo kikuu cha maji kwa ajili ya mji wa Port Sudan, unaokaliwa na watu wanaofanya shughuli zao kwenye bandari ya Bahari ya Shamu, na uwanja wa ndege, na kupokea misaada inayohitajika sana kwa ajili ya watu wa Sudan.

Timu ya serikali iliyoundwa kwa ajili ya kuthathmini athari ya mvua ilisema Jumatatu kwamba watu 132 wameuawa katika mfuriko kote Sudan na Umoja wa Mataifa umesema kwamba wengine 118,000 wamekoseshwa makazi.

Forum

XS
SM
MD
LG