Serikali ya Tanzania siku ya Alhamisi, imetangaza kumalizika kwa mlipuko wa ugonjwa wa Marburg baada ya siku 42 bila kuwepo na maambukizi mapya, hatua inayokidhi vigezo vya Shirika la Afya Duniani (WHO).
Wizara ya Afya nchini Tanzania Jumatatu imesema kuwa watu wawili (2) wamegundulika kuwa na maambukizi ya virusi vinavyosababisha ugonjwa wa Mpox.
Tanzania imeungana na mataifa mengine ulimwenguni kusheherekea Siku ya Kimataifa ya Wanawake, maadhimisho ya kitaifa yakifanyika mkoani Arusha. Katika maadhimisho hayo, wanawake wameitaka serikali kuendelea kuboresha huduma za afya, hasa kwa wanawake wenye umri mkubwa.
Katika hatua mpya ya kutafuta amani mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), viongozi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki(EAC) na Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC) wamefikia maamuzi yatakayosaidia kurejesha utulivu katika eneo hilo linalokumbwa namzozo wa muda mrefu.
Rais wa Rwanda, Paul Kagame, na mwenzake wa Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Felix Tshisekedi, walishiriki mkutano wa Jumamosi, Tanzania, ambapo viongozi wa kikanda walitoa mwito wa kusitishwa mara moja kwa mapigano nchini DRC.
Rwanda Jumapili imekubaliana na pendekezo la kufanyika kwa mkutano utakaosimamiwa na SADC na Jumuia ya Afrika Mashariki kujadili mzozo wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, huku Tanzania ikitangaza pia kwamba wanajeshi wake wawili waliuawa katika mapigano ya hivi karibuni.
Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ), Jumapili limesema wanajeshi wake wawili wameuawa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC).
Jumuia ya Afrika Mashariki Jumatano imeitaka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kuzungumza na “wadau wote”, wakiwemo wapiganaji wanaoungwa mkono na Rwanda, ili kumaliza mapigano katika eneo la mashariki mwa nchi.
Chama kikuu cha upinzani nchini Tanzania kimefanya uchaguzi mkuu na kumchagua kiongozi mpya kabla ya uchaguzi mkuu wa taifa mwezi Oktoba mwaka huu wakati ambapo chama kinakabiliwa na ongezeko la ukandamizaji wa kisiasa.
Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan Jumatatu alithibitisha uwepo wa mlipuko hatari wa virusi vya Marburg kaskazini magharibi mwa nchi, huku kesi nyingine moja ya ugonjwa huo ikiripotiwa.
Shirika la afya duniani WHO Jumanne limesema kwamba mlipuko unaoshukiwa wa ugonjwa hatari wa Marburg nchini Tanzania umewaua watu wanane, na kuonya kwamba hatari ya kusambaa kwa ugonjwa huo nchini humo ni “kubwa”.
Mwanahabari na mwanaharakati Maria Sarungi hatimaye amevunja ukimya kufuatia jaribio la kumteka nyara siku ya jumapili Nairobi, Kenya
Pandisha zaidi