Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatatu, Julai 01, 2024 Local time: 20:04

Wamauritania wafanya uchaguzi huku Rais Ghazouani akitarajiwa kushinda


Bango la Rais Mohamed Ould Ghazouani.
Bango la Rais Mohamed Ould Ghazouani.

Raia wa Mauritania walipiga kura siku ya Jumamosi katika uchaguzi wa rais ambao kiongozi wa sasa wa nchi hiyo, Mohamed Ould Ghazouani, anatarajiwa kushinda.

Mwanasiasa huyo ameahidi kuimarisha uwekezaji katika nchi hiyo ya Afrika Magharibi inapojiandaa kuanza uzalishaji wa gesi asilia.

Ghazouani, mwenye umri wa miaka 67, ambaye zamani alikuwa afisa mwandamizi wa kijeshi, ameahidi sera rafiki kwa wawekezaji ili kuchochea ukuaji wa bidhaa katika nchi hiyo yenye watu milioni 5, ambao wengi wao wanaishi katika umaskini licha ya utajiri wake wa mafuta na madini.

"Neno la mwisho ni la wapiga kura wa Mauritania. Ninajitolea kuheshimu chaguo lao," Ghazouani alisema baada ya kupiga kura katika mji mkuu.

Vituo vya kupigia kura vilifunguliwa saa moja asubuhi saa za huko, na zoezi hilo lilitarajiwa kumalizika saa moja jioni, huku matokeo ya awali yakitarajiwa kuanzia Jumapili.

Ghazouani alichaguliwa kwa muhula wa kwanza mnamo 2019, na anakabiliana na wapinzani sita, kati yao akiwa ni mwanaharakati wa kupinga utumwa, Biram Dah Abeid, ambaye aliibuka wa pili katika uchaguzi wa mwaka 2019 kwa kupata zaidi ya asili mia 18 ya kura.

Forum

XS
SM
MD
LG