Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatatu, Septemba 16, 2024 Local time: 13:00

Japan yatoa tahadhari cha Kimbunga Shanshan


High waves are observed along the shore as Typhoon Shanshan approaches southwestern Japan in Ibusuki, Kagoshima Prefecture, Aug. 28, 2024, in this photo taken by Kyodo.
High waves are observed along the shore as Typhoon Shanshan approaches southwestern Japan in Ibusuki, Kagoshima Prefecture, Aug. 28, 2024, in this photo taken by Kyodo.

Japan ilikuwa ikijiandaa kukabiliana na kimbunga chenye nguvu huku kikikaribia polepole kusini-magharibi mwa nchi hiyo.

Kimbunga kicho chenye mwendo wa kasi kinatishia kusababisha mvua kubwa na upepo mkali na kuyafanya mashirika ya ndege kusitisha safari za ndege na huduma za usafiri wa treni.

Pia mashirika hayo yametakiwa kuchelewesha safari au kusimamisha huduma hadi mwishoni mwa juma.

Kimbunga Shanshan kilikuwa takriban kilomita 120 kusini mwa kisiwa cha Yakushima leo asubuhi kilipokuwa kikielekea kaskazini kuelekea Kyushu, kikipakia upepo wa hadi kilomita 180 kwa saa, kulingana na Shirika la Hali ya Hewa la Japan.

Shirika hilo lilisema kimbunga hicho kinatarajiwa kufika Kyushu kusini na ikiwezekana kutua Alhamisi, na kutoa onyo la hali ya juu dhidi ya upepo mkali, mawimbi makubwa na mvua kubwa katika mkoa wa Kagoshima.

Mashirika mengi ya Ndege zenye huduma za ndani ya nchi zinazounganisha miji na visiwa vya kusini-magharibi zitasitishwa hadi Ijumaa.

Huduma za posta na utoaji pia zimesitishwa katika eneo la Kyushu, na maduka makubwa na maduka mengine yalitangaza mipango ya kufungwa mapema.

Forum

XS
SM
MD
LG