Waziri wa mambo ya nje wa marekani Marco Rubio amezungumza na waziri wa mambo ya nje wa Angola Tete antoniuo jana kuhusu kubuni njia ya kuumaliza kwa amani mzozo wa mashariki mwa DRC , Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani imesema.
Taarifa hiyo imeongeza kusema kuwa “ Waziri Rubio na Waziri wa Mambo ya Nje Antonio wamejadili kuhusu mchakato wa Luanda na uongozi wa Angola kufanyakazi kutafuta suluhisho la amani kwa mzozo wa mashariki mwa DRC.”
Hata hivyo Washington imeonya kuhusu uwezekano wa kuweka vikwazo dhidi ya maafisa wa Rwanda na Congo kutokana na mzozo huo.
Rais wa Rwanda Paul Kagame
Kuhusu waraka wa kidiplomasia ambao Reuters imeuona mapema mwezi huu , Marekani ilisema kwamba utulivu katika eneo unataka jeshi la Rwanda kuondoa vikosi vyake na silaha za hali ya juu kutoka DRC.