Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatatu, Machi 31, 2025 Local time: 05:48

Waumini wamuombea Papa Francis wakati akiwa mahututi hospitali


Watu waliohudhiria maombi huko St. Peter's Square, wakati papa rancis akiwa nado hospitali huko Vatican, February 25, 2025. Picha na REUTERS
Watu waliohudhiria maombi huko St. Peter's Square, wakati papa rancis akiwa nado hospitali huko Vatican, February 25, 2025. Picha na REUTERS

Waumini wamekusanyika huko Saint Peters Square na nje ya hospitali ya Gemelli siku ya Jumanne wakati Papa Francis akiwa bado katika hali mahututi.

Papa amekutana na viongozi wenzake wakuu akiwa hospitali kujadili masuala ya kazi, Vatican imesema siku ya Jumanne, na maafisa wamesema alikuwa akila kama kawaida na anatembea.

Papa mwenye umri wa miaka 88 amekuwa katika hopitali ya Rome ya Gemelli kwa siku ya 12, muda mrefu kwa papa kulazwa hospitali katika miaka yake 12 ya upapa.

Afisa wa Vatican, ambaye hakutaka jina lake litajwe kwa sababu hakuwa na mamlaka ya kujadili hali ya papa, amesema Francis anakula kama kawaida, anatembea katika chumba chake cha hospital, na anaendelea na matibabu.

Vatican imesema Francis amekutana na kadinali Pietro Parolin wa pili anayemfuatia katika safu yake na naibu wa Parolin siku ya Jumatatu.

Forum

XS
SM
MD
LG