Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Julai 06, 2024 Local time: 04:23

Wagombe urais Senegal wasusia mazungumzo yaliyopendekezwa na Rais Sall


Watu wakimtazama rais Macky Sall wakati wa mkutano na waandishi wa habari uliotangazwa moja kwa moja na televisheni ya taifa . Picha na Michele Cattani / AFP
Watu wakimtazama rais Macky Sall wakati wa mkutano na waandishi wa habari uliotangazwa moja kwa moja na televisheni ya taifa . Picha na Michele Cattani / AFP

Wagombea wengi katika uchaguzi ulioahirishwa nchini Senegal na kundi kubwa la jumuiya za kiraia kwa pamoja wamesema siku ya Ijumaa kuwa, hawatashiriki katika mazungumzo yaliyopendekezwa na Rais Macky Sall kuamua tarehe ya upigaji kura ambao aliuahirisha mapema mwezi huu.

Sall anapamba na ongezeko la wito wa kumtaka atangaze siku ya uchaguzi wa rais baada ya kuuahirisha ghafla uchaguzi wa Februari 25 na kusababisha mgogoro wa kisiasa kwa wiki kadhaa.

Lakini katika majojiano ya television siku ya Alhamisi jioni, hakuzungumzia uamuzi wa kutaja tarehe mpaka baada ya mazungumzo na wanasiasa na watendaji wa kijamii, yanayotarajiwa kuanza Jumatatu.

Amesema anatarajia kufikia makubaliano ifikapo Junanne jioni.

“Tunapinga mapendekezo ya mdahalo na tunataka tarehe ipangwe kabla ya Aprili 2” Boubacar Camara mmoja wa kundi hilo la wagombea 16 aliwaambia waandishi wa habari siku ya Ijumaa.

Sall alisisitiza wakati alipoonekaka kwenye televisheni kuwa mamlaka yake itafikia hatima ya uongozi wake kama ilivyopangwa tarehe 2 Aprili.

Lakini alicha wazi swali la ni lini uchaguzi huo utafanyika. Alipobanwa , aliongeza kuwa hafikirii kama itawezekana kufanyika kabla ya April 2. Chanzo cha habari hii ni shirika la habari la AFP

Forum

XS
SM
MD
LG