Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Septemba 20, 2024 Local time: 02:07

Trump akosoa Harris anavyo shughulikia usalama mpakani kati ya Marekani-Mexico


Rais wa zamani Donald Trump ( wa tatu kutoka kushoto) azuru mpaka wa Marekani na Mexico huko katika Kaunti ya Cochise, Arizona.
Rais wa zamani Donald Trump ( wa tatu kutoka kushoto) azuru mpaka wa Marekani na Mexico huko katika Kaunti ya Cochise, Arizona.

“Kamwe hakujawahi kuwa na mpaka kokote duniani ambao unafurika watu kama mpaka huu.”

Harris alipewa jukumu mwezi Machi 2021 kukabiliana na “kiini” cha wahamiaji kutoka Guatemala, Honduras na El Salvador – Amerika ya Kati inayoitwa “Northern Triangle” – lakini haikupewa jina la “border czar” au kupewa jukumu la ulinzi wa mpaka.

Kwenye barabara chafu chini ya vilima vyenye vichaka vya Arizona, Donald Trump alitumia ukuta na rundo la vyuma kulinganisha jinsi yeye alivyoudhibiti mpaka huo na hatua za mpinzani wake Mdemokrat, Makamu wa Rais Kamala Harris.

Trump aliwaleta wanawake wenye huzuni, mkuu wa polisi wa Kaunti ya Cochise na mkuu wa umoja wa Doria ya Mpakani kupeleka ujumbe wake mzito juu ya ulinzi wa mpaka katika ziara yake Alhamisi, iliyopewa kauli mbiu “Make America Safe Again” (Ifanye Marekani Iwe Salama Tena.)

Kabla ya matamshi yake, Trump alianza kwa kukosoa rekodi ya Harris kuhusu uhamiaji na usalama wa mpakani, akimuita “makamu wa rais ovyo” alipokuwa anazunguka na kuzungumza na wakazi wa eneo karibu na uzio wa mpaka.

Forum

XS
SM
MD
LG