Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumapili, Aprili 06, 2025 Local time: 22:44

Rubio kutohudhuria mkutano wa mawaziri wa mambo ya nje wa G20


Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Marco Rubio.
Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Marco Rubio.

Mwanadiplomasia wa juu wa Marekani Marco Rubio hatohudhuria Mkutano wa mawaziri wa mambo ya nje wa G20 utakaofanyika Afrika kusini wiki hii huku kukiwa na mivutano inayoendelea baina ya mataifa hayo mawili.

Huu ni Mkutano wa kwanza wa mawaziri wa mambo ya nje kutoka kundi la G20 yenye Uchumi mkubwa tangu Afrika kusini ilipochukua nafasi ya urais Desemba mwaka jana.

Uhusiano wa kidiplomasia baina ya Pretoria na Washington chini ya utawala mpya wa rais Donald Trump umekuwa na Dosari.

Rais wa Marekani Donald Trump (kushoto) na Rais wa Afrika Kusini Cyril Ramaphosa.
Rais wa Marekani Donald Trump (kushoto) na Rais wa Afrika Kusini Cyril Ramaphosa.

Trump amekata misaada katika serikali inayoongozwa na watu Weusi ya Afrika Kusini kufuatia amri yake ya kiutendaji wiki iliyopita.

Katika agizo hilo Trump alisema waafrika kusini ambao ni walowezi wa kikoloni wa uholanzi walikuwa wanalengwa na sheria mpya inayoruhusu serikali kunyakua ardhi binafsi.

Forum

XS
SM
MD
LG