Waziri wa Ulinzi wa Israel atembelea Marekani kuzungumzia vita vya Gaza

  • VOA News

Waziri wa Ulinzi wa Israel Yoav Gallant .March 26, 2024.

Waziri wa Ulinzi wa Israel Yoav Gallant, Jumapili ametembelea Washington, ili kuzungumzia kuhusu awamu nyingine ya vita vya Gaza, pamoja na ghasia zinazoendelea kwenye mpaka wa Israel na Lebanon, ambako makabiliano na wapiganaji wa Hezbollah, yamezua wasi wasi wa kuongozeka kwa ghasia hizo.

Kundi la Hezbollah linaloungwa mkono na Iran limekuwa likishambuliana na Israel, tangu kuzuka kwa vita vya Gaza miezi 8 iliopita, likisema kuwa halitasitisha mashambulizi hadi pale kutakapokuwa na sitisho la mapigano huko Gaza.

Kabla ya kuanza safari yake ya Washingon, Gallant kupitia taarifa amesema kwamba wapo tayari kwa hatua yoyote inayohitajika huko Gaza, Lebanon na maeneo mengine. Mapema mwezi huu Hezbollah walilenga miji kadhaa ya Israel, pamoja na vituo vya kijeshi, baada ya Israel kuuwa kamanda wa ngazi ya juu zaidi wa kundi hilo.

Mjumbe wa Marekani Amos Hochstein wiki iliopita alitembelea Lebanon na Israel, akijaribu kupunguza mzozo uliopo kwenye mpaka wa mataifa hayo. Baadhi ya maafisa wa Israel wameashiria kuwa huenda Israel ikalenga Lebanon, baada ya mashambulizi ya mji wa kusini mwa Gaza wa Rafah yanayosemekana kulenga kundi la mwisho la wapiganaji wa Hamas.