Waafrika waombwa kuchukua jukumu la kuendeleza sinema zao

Muigizaji wa Uingereza Idris Elba (kushoto) akiwa na mkewe mwanamitindo Sabrina Elba walipowasili katika tunzo za Emmy hulo Los Angeles Septemba 15, 2024. Picha na Michael TRAN / AFP.

Mcheza sinema wa Uingereza Idris Elba amesema mustakabali wa sinema za Kiafrika “unategemea” mtazamo wa kwanza wa Afrika.

Amesema wakati alipokuwa amehudhuria tukio la kwanza la filamu, mkutano wa kwanza wa filamu wa Afrika katika mji mkuu wa Ghana, Accra.

Ni vizuri kuwa tunaona ongezeko la filamu za Afrika kwenye Netflix, na kwenye Prime na nyinginezo. Lakini mustakabali wa utengenezaji wa filamu uko mikononi mwetu, na siyo majukwaa hayo”.

Anasema mwigizaji na mshindi wa tuzo ya Golden Globe aliyezaliwa na baba raia wa Ghana na mama raia wa Sierra Leone.

“Tunatakiwa tuwe na usambazaji, lazima tuwe na muunganisho, tunapaswa tuwe na sinema, kile ninachokiita msisimko kwenye viti.