Marekani: Fahamu namna Chama cha Republikan kinavyochagua wagombea wa urais

Your browser doesn’t support HTML5

Januari 15, msimu wa uchaguzi wa rais Marekani 2024 utazinduliwa rasmi kwa mikutano ya vyama ya kuchagua wagombea huko Iowa.

Wagombea wa chama cha Republikan akiwemo Ron DeSantis, Nikki Haley, na Vivek Ramaswamy wanataka kumuondoa Rais wa zamani Donald Trump ambaye ni mgombea mkuu, hatimaye kuwa mgombea wa chama hicho kukabiliana na Rais aliyeko madarakani Joe Biden katika uchaguzi mkuu wa Novemba 2024.

Endelea kusikiliza ripoti kamili ya maelezo kuhusu mikutano ya vyama ya kuchagua wagombea huko Iowa, Marekani