Biden na Trump watafuta kura za wanawake

Your browser doesn’t support HTML5

Wapiga kura wanawake ni zaidi ya nusu ya wapigakura wote hapa Marekani na katika uchaguzi wa mwaka 2024 kura zao zimekua muhimu kwa wagombea kiti cha rais hawa kutokana na suala la utuaji mimba na haki za uzazi.

Sehemu kubwa ya kampeni za urais zinalenga wapiga kura wanawake hasa katika suala la sheria ya utoaji mimba na haki ya uzazi. Lakini wanawake wa Marekani wanajali sana masuala mengine na siyo tu utoaji mimba, nkampeni zinawafikia kwa masuala mengine ikiwemo uchumi, huduma za afya na uhalifu.